< Zaburi 91 >

1 Yeye akaaye mahali pa salama pake Yeye Aliye Juu Sana, atadumu katika uvuli wake Mwenyezi.
Celui qui habite dans la [demeure] secrète du Très-haut logera à l’ombre du Tout-puissant.
2 Nitasema kumhusu Bwana, “Yeye ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye ninamtumaini.”
J’ai dit de l’Éternel: Il est ma confiance et mon lieu fort; il est mon Dieu, je me confierai en lui.
3 Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji, na maradhi ya kuambukiza ya kuua.
Car il te délivrera du piège de l’oiseleur, de la peste calamiteuse.
4 Atakufunika kwa manyoya yake, chini ya mbawa zake utapata kimbilio, uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.
Il te couvrira de ses plumes, et sous ses ailes tu auras un refuge; sa vérité sera ton bouclier et ta rondache.
5 Hutaogopa vitisho vya usiku, wala mshale urukao mchana,
Tu n’auras pas peur des frayeurs de la nuit, ni de la flèche qui vole de jour,
6 wala maradhi ya kuambukiza yanayonyemelea gizani, wala tauni iharibuyo adhuhuri.
Ni de la peste qui marche dans les ténèbres, ni de la destruction qui dévaste en plein midi.
7 Ijapo watu elfu wataangukia kando yako, kumi elfu mkono wako wa kuume, lakini haitakukaribia wewe.
Il en tombera mille à ton côté, et dix mille à ta droite; – toi, tu ne seras pas atteint.
8 Utatazama tu kwa macho yako na kuona adhabu ya waovu.
Seulement tu contempleras de tes yeux, et tu verras la récompense des méchants.
9 Kama ukimfanya Aliye Juu Sana kuwa makao yako: naam, Bwana ambaye ni kimbilio langu,
Parce que toi tu as mis l’Éternel, mon refuge, le Très-haut, pour ta demeure,
10 basi hakuna madhara yatakayokupata wewe, hakuna maafa yataikaribia hema yako.
Aucun mal ne t’arrivera, et aucune plaie n’approchera de ta tente;
11 Kwa kuwa atawaagiza malaika zake kwa ajili yako, wakulinde katika njia zako zote.
Car il commandera à ses anges à ton sujet, de te garder en toutes tes voies:
12 Mikononi mwao watakuinua, ili usijikwae mguu wako kwenye jiwe.
Ils te porteront sur leurs mains, de peur que tu ne heurtes ton pied contre une pierre.
13 Utawakanyaga simba na nyoka wakali, simba mkubwa na nyoka utawaponda kwa miguu.
Tu marcheras sur le lion et sur l’aspic, tu fouleras le lionceau et le dragon.
14 Bwana asema, “Kwa kuwa ananipenda, nitamwokoa; nitamlinda, kwa kuwa analikiri Jina langu.
Parce qu’il a mis son affection sur moi, je le délivrerai; je le mettrai en une haute retraite, parce qu’il a connu mon nom.
15 Ataniita, nami nitamjibu; nitakuwa pamoja naye katika taabu, nitamwokoa na kumheshimu.
Il m’invoquera, et je lui répondrai; dans la détresse je serai avec lui; je le délivrerai et le glorifierai.
16 Kwa siku nyingi nitamshibisha na kumwonyesha wokovu wangu.”
Je le rassasierai de longs jours, et je lui ferai voir mon salut.

< Zaburi 91 >