< Zaburi 91 >

1 Yeye akaaye mahali pa salama pake Yeye Aliye Juu Sana, atadumu katika uvuli wake Mwenyezi.
Celui qui s'abrite sous la protection du Très-Haut repose à l'ombre du Tout-Puissant.
2 Nitasema kumhusu Bwana, “Yeye ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye ninamtumaini.”
Je dis à Yahweh: " Tu es mon refuge et ma forteresse, mon Dieu en qui je me confie. "
3 Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji, na maradhi ya kuambukiza ya kuua.
Car c'est lui qui te délivre du filet de l'oiseleur et de la peste funeste.
4 Atakufunika kwa manyoya yake, chini ya mbawa zake utapata kimbilio, uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.
Il te couvrira de ses ailes, et sous ses plumes tu trouveras un refuge. Sa fidélité est un bouclier et une cuirasse.
5 Hutaogopa vitisho vya usiku, wala mshale urukao mchana,
Tu n'auras à craindre ni les terreurs de la nuit, ni la flèche qui vole pendant le jour,
6 wala maradhi ya kuambukiza yanayonyemelea gizani, wala tauni iharibuyo adhuhuri.
ni la peste qui marche dans les ténèbres, ni la contagion qui ravage en plein midi.
7 Ijapo watu elfu wataangukia kando yako, kumi elfu mkono wako wa kuume, lakini haitakukaribia wewe.
Que mille tombent à ton côté, et dix mille à ta droite, tu ne seras pas atteint.
8 Utatazama tu kwa macho yako na kuona adhabu ya waovu.
De tes yeux seulement tu regarderas, et tu verras la rétribution des méchants.
9 Kama ukimfanya Aliye Juu Sana kuwa makao yako: naam, Bwana ambaye ni kimbilio langu,
Car tu as dit: " Tu es mon refuge, Yahweh! " tu as fait du Très-Haut ton asile.
10 basi hakuna madhara yatakayokupata wewe, hakuna maafa yataikaribia hema yako.
Le malheur ne viendra pas jusqu'à toi, aucun fléau n'approchera de ta tente.
11 Kwa kuwa atawaagiza malaika zake kwa ajili yako, wakulinde katika njia zako zote.
Car il ordonnera à ses anges de te garder dans toutes tes voies.
12 Mikononi mwao watakuinua, ili usijikwae mguu wako kwenye jiwe.
Ils te porteront sur leurs mains, de peur que ton pied ne heurte contre la pierre.
13 Utawakanyaga simba na nyoka wakali, simba mkubwa na nyoka utawaponda kwa miguu.
Tu marcheras sur le lion et sur l'aspic, tu fouleras le lionceau et le dragon. —
14 Bwana asema, “Kwa kuwa ananipenda, nitamwokoa; nitamlinda, kwa kuwa analikiri Jina langu.
" Puisqu'il s'est attaché à moi, je le délivrerai; je le protégerai, puisqu'il connaît mon nom.
15 Ataniita, nami nitamjibu; nitakuwa pamoja naye katika taabu, nitamwokoa na kumheshimu.
Il m'invoquera et je l'exaucerai; je serai avec lui dans la détresse. " Je le délivrerai et le glorifierai.
16 Kwa siku nyingi nitamshibisha na kumwonyesha wokovu wangu.”
Je le rassasierai de longs jours, et je lui ferai voir mon salut. "

< Zaburi 91 >