< Zaburi 91 >

1 Yeye akaaye mahali pa salama pake Yeye Aliye Juu Sana, atadumu katika uvuli wake Mwenyezi.
He that dwellith in the help of the hiyeste God; schal dwelle in the proteccioun of God of heuene.
2 Nitasema kumhusu Bwana, “Yeye ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye ninamtumaini.”
He schal seie to the Lord, Thou art myn vptaker, and my refuit; my God, Y schal hope in him.
3 Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji, na maradhi ya kuambukiza ya kuua.
For he delyuered me fro the snare of hunteris; and fro a scharp word.
4 Atakufunika kwa manyoya yake, chini ya mbawa zake utapata kimbilio, uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.
With hise schuldris he schal make schadowe to thee; and thou schalt haue hope vnder hise fetheris.
5 Hutaogopa vitisho vya usiku, wala mshale urukao mchana,
His treuthe schal cumpasse thee with a scheld; thou schalt not drede of nyytis drede.
6 wala maradhi ya kuambukiza yanayonyemelea gizani, wala tauni iharibuyo adhuhuri.
Of an arowe fliynge in the dai, of a gobelyn goynge in derknessis; of asailing, and a myddai feend.
7 Ijapo watu elfu wataangukia kando yako, kumi elfu mkono wako wa kuume, lakini haitakukaribia wewe.
A thousynde schulen falle doun fro thi side, and ten thousynde fro thi riytside; forsothe it schal not neiye to thee.
8 Utatazama tu kwa macho yako na kuona adhabu ya waovu.
Netheles thou schalt biholde with thin iyen; and thou schalt se the yelding of synneris.
9 Kama ukimfanya Aliye Juu Sana kuwa makao yako: naam, Bwana ambaye ni kimbilio langu,
For thou, Lord, art myn hope; thou hast set thin help altherhiyeste.
10 basi hakuna madhara yatakayokupata wewe, hakuna maafa yataikaribia hema yako.
Yuel schal not come to thee; and a scourge schal not neiye to thi tabernacle.
11 Kwa kuwa atawaagiza malaika zake kwa ajili yako, wakulinde katika njia zako zote.
For God hath comaundid to hise aungels of thee; that thei kepe thee in alle thi weies.
12 Mikononi mwao watakuinua, ili usijikwae mguu wako kwenye jiwe.
Thei schulen beere thee in the hondis; leste perauenture thou hirte thi foot at a stoon.
13 Utawakanyaga simba na nyoka wakali, simba mkubwa na nyoka utawaponda kwa miguu.
Thou schalt go on a snake, and a cocatrice; and thou schalt defoule a lioun and a dragoun.
14 Bwana asema, “Kwa kuwa ananipenda, nitamwokoa; nitamlinda, kwa kuwa analikiri Jina langu.
For he hopide in me, Y schal delyuere hym; Y schal defende him, for he knew my name.
15 Ataniita, nami nitamjibu; nitakuwa pamoja naye katika taabu, nitamwokoa na kumheshimu.
He criede to me, and Y schal here him, Y am with him in tribulacioun; Y schal delyuere him, and Y schal glorifie hym.
16 Kwa siku nyingi nitamshibisha na kumwonyesha wokovu wangu.”
I schal fille hym with the lengthe of daies; and Y schal schewe myn helthe to him.

< Zaburi 91 >