< Zaburi 91 >

1 Yeye akaaye mahali pa salama pake Yeye Aliye Juu Sana, atadumu katika uvuli wake Mwenyezi.
He who dwells in the secret place of the Most High will rest in the shadow of Shaddai.
2 Nitasema kumhusu Bwana, “Yeye ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye ninamtumaini.”
I will say of Jehovah, "He is my refuge and my fortress; my God, in whom I trust."
3 Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji, na maradhi ya kuambukiza ya kuua.
For he will deliver you from the snare of the fowler, and from the deadly pestilence.
4 Atakufunika kwa manyoya yake, chini ya mbawa zake utapata kimbilio, uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.
He will cover you with his feathers. Under his wings you will take refuge. His truth is an encompassing shield.
5 Hutaogopa vitisho vya usiku, wala mshale urukao mchana,
You shall not be afraid of the terror by night, nor of the arrow that flies by day;
6 wala maradhi ya kuambukiza yanayonyemelea gizani, wala tauni iharibuyo adhuhuri.
nor of the pestilence that walks in darkness, nor of the destruction that wastes at noonday.
7 Ijapo watu elfu wataangukia kando yako, kumi elfu mkono wako wa kuume, lakini haitakukaribia wewe.
A thousand may fall at your side, and ten thousand at your right hand; but it will not come near you.
8 Utatazama tu kwa macho yako na kuona adhabu ya waovu.
You will only look with your eyes, and see the recompense of the wicked.
9 Kama ukimfanya Aliye Juu Sana kuwa makao yako: naam, Bwana ambaye ni kimbilio langu,
Because you have made Jehovah your refuge, and the Most High your dwelling place,
10 basi hakuna madhara yatakayokupata wewe, hakuna maafa yataikaribia hema yako.
no evil shall overtake you; no plague shall come near your dwelling.
11 Kwa kuwa atawaagiza malaika zake kwa ajili yako, wakulinde katika njia zako zote.
For he will put his angels in charge of you, to guard you in all your ways.
12 Mikononi mwao watakuinua, ili usijikwae mguu wako kwenye jiwe.
In their hands they will lift you up, so that you will not strike your foot against a stone.
13 Utawakanyaga simba na nyoka wakali, simba mkubwa na nyoka utawaponda kwa miguu.
You will tread upon the lion and the viper. You will trample the young lion and the serpent underfoot.
14 Bwana asema, “Kwa kuwa ananipenda, nitamwokoa; nitamlinda, kwa kuwa analikiri Jina langu.
"Because he has set his love on me, therefore I will deliver him. I will set him on high, because he has known my name.
15 Ataniita, nami nitamjibu; nitakuwa pamoja naye katika taabu, nitamwokoa na kumheshimu.
He will call on me, and I will answer him. I will be with him in trouble. I will deliver him, and honor him.
16 Kwa siku nyingi nitamshibisha na kumwonyesha wokovu wangu.”
I will satisfy him with long life, and show him my salvation."

< Zaburi 91 >