< Zaburi 91 >

1 Yeye akaaye mahali pa salama pake Yeye Aliye Juu Sana, atadumu katika uvuli wake Mwenyezi.
He who is dwelling In the secret place of the Most High, Habitually lodges in the shade of the Mighty,
2 Nitasema kumhusu Bwana, “Yeye ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye ninamtumaini.”
He is saying of YHWH, “My refuge, and my bulwark, my God, I trust in Him,”
3 Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji, na maradhi ya kuambukiza ya kuua.
For He delivers you from the snare of a fowler, From a calamitous pestilence.
4 Atakufunika kwa manyoya yake, chini ya mbawa zake utapata kimbilio, uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.
He covers you over with His pinion, And under His wings you trust, His truth [is] a shield and buckler.
5 Hutaogopa vitisho vya usiku, wala mshale urukao mchana,
You are not afraid of fear by night, Of arrow that flies by day,
6 wala maradhi ya kuambukiza yanayonyemelea gizani, wala tauni iharibuyo adhuhuri.
Of pestilence that walks in thick darkness, Of destruction that destroys at noon,
7 Ijapo watu elfu wataangukia kando yako, kumi elfu mkono wako wa kuume, lakini haitakukaribia wewe.
One thousand fall at your side, And a myriad at your right hand, [But] it does not come near to you.
8 Utatazama tu kwa macho yako na kuona adhabu ya waovu.
But with your eyes you look, And you see the reward of the wicked,
9 Kama ukimfanya Aliye Juu Sana kuwa makao yako: naam, Bwana ambaye ni kimbilio langu,
(For You, O YHWH, [are] my refuge), You made the Most High your habitation.
10 basi hakuna madhara yatakayokupata wewe, hakuna maafa yataikaribia hema yako.
Evil does not happen to you, And a plague does not come near your tent,
11 Kwa kuwa atawaagiza malaika zake kwa ajili yako, wakulinde katika njia zako zote.
For He charges His messengers for you, To keep you in all your ways,
12 Mikononi mwao watakuinua, ili usijikwae mguu wako kwenye jiwe.
On the hands they bear you up, Lest you strike your foot against a stone.
13 Utawakanyaga simba na nyoka wakali, simba mkubwa na nyoka utawaponda kwa miguu.
You tread on lion and cobra, You trample young lion and dragon.
14 Bwana asema, “Kwa kuwa ananipenda, nitamwokoa; nitamlinda, kwa kuwa analikiri Jina langu.
Because he has delighted in Me, I also deliver him—I set him on high, Because he has known My Name.
15 Ataniita, nami nitamjibu; nitakuwa pamoja naye katika taabu, nitamwokoa na kumheshimu.
He calls Me, and I answer him, I [am] with him in distress, I deliver him, and honor him.
16 Kwa siku nyingi nitamshibisha na kumwonyesha wokovu wangu.”
I satisfy him with [the] length of [his] days, And I cause him to look on My salvation!

< Zaburi 91 >