< Zaburi 91 >

1 Yeye akaaye mahali pa salama pake Yeye Aliye Juu Sana, atadumu katika uvuli wake Mwenyezi.
O thou that dwellest in the covert of the Most High, and abidest in the shadow of the Almighty;
2 Nitasema kumhusu Bwana, “Yeye ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye ninamtumaini.”
I will say of the LORD, who is my refuge and my fortress, my God, in whom I trust,
3 Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji, na maradhi ya kuambukiza ya kuua.
That He will deliver thee from the snare of the fowler, and from the noisome pestilence.
4 Atakufunika kwa manyoya yake, chini ya mbawa zake utapata kimbilio, uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.
He will cover thee with His pinions, and under His wings shalt thou take refuge; His truth is a shield and a buckler.
5 Hutaogopa vitisho vya usiku, wala mshale urukao mchana,
Thou shalt not be afraid of the terror by night, nor of the arrow that flieth by day;
6 wala maradhi ya kuambukiza yanayonyemelea gizani, wala tauni iharibuyo adhuhuri.
Of the pestilence that walketh in darkness, nor of the destruction that wasteth at noonday.
7 Ijapo watu elfu wataangukia kando yako, kumi elfu mkono wako wa kuume, lakini haitakukaribia wewe.
A thousand may fall at Thy side, and ten thousand at Thy right hand; it shall not come nigh thee.
8 Utatazama tu kwa macho yako na kuona adhabu ya waovu.
Only with thine eyes shalt thou behold, and see the recompense of the wicked.
9 Kama ukimfanya Aliye Juu Sana kuwa makao yako: naam, Bwana ambaye ni kimbilio langu,
For thou hast made the LORD who is my refuge, even the Most High, thy habitation.
10 basi hakuna madhara yatakayokupata wewe, hakuna maafa yataikaribia hema yako.
There shall no evil befall thee, neither shall any plague come nigh thy tent.
11 Kwa kuwa atawaagiza malaika zake kwa ajili yako, wakulinde katika njia zako zote.
For He will give His angels charge over thee, to keep thee in all thy ways.
12 Mikononi mwao watakuinua, ili usijikwae mguu wako kwenye jiwe.
They shall bear thee upon their hands, lest thou dash thy foot against a stone.
13 Utawakanyaga simba na nyoka wakali, simba mkubwa na nyoka utawaponda kwa miguu.
Thou shalt tread upon the lion and asp; the young lion and the serpent shalt thou trample under feet.
14 Bwana asema, “Kwa kuwa ananipenda, nitamwokoa; nitamlinda, kwa kuwa analikiri Jina langu.
'Because he hath set his love upon Me, therefore will I deliver him; I will set him on high, because he hath known My name.
15 Ataniita, nami nitamjibu; nitakuwa pamoja naye katika taabu, nitamwokoa na kumheshimu.
He shall call upon Me, and I will answer him; I will be with him in trouble; I will rescue him, and bring him to honour.
16 Kwa siku nyingi nitamshibisha na kumwonyesha wokovu wangu.”
With long life will I satisfy him, and make Him to behold My salvation.'

< Zaburi 91 >