< Zaburi 91 >
1 Yeye akaaye mahali pa salama pake Yeye Aliye Juu Sana, atadumu katika uvuli wake Mwenyezi.
He that dwelleth in the secret place of the Most High shall abide under the shadow of the Almighty.
2 Nitasema kumhusu Bwana, “Yeye ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye ninamtumaini.”
I say of Jehovah, My refuge and my fortress; my God, I will confide in him.
3 Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji, na maradhi ya kuambukiza ya kuua.
Surely he shall deliver thee from the snare of the fowler, [and] from the destructive pestilence.
4 Atakufunika kwa manyoya yake, chini ya mbawa zake utapata kimbilio, uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.
He shall cover thee with his feathers, and under his wings shalt thou find refuge: his truth is a shield and buckler.
5 Hutaogopa vitisho vya usiku, wala mshale urukao mchana,
Thou shalt not be afraid for the terror by night, for the arrow that flieth by day,
6 wala maradhi ya kuambukiza yanayonyemelea gizani, wala tauni iharibuyo adhuhuri.
For the pestilence that walketh in darkness, for the destruction that wasteth at noonday.
7 Ijapo watu elfu wataangukia kando yako, kumi elfu mkono wako wa kuume, lakini haitakukaribia wewe.
A thousand shall fall at thy side, and ten thousand at thy right hand; [but] it shall not come nigh thee.
8 Utatazama tu kwa macho yako na kuona adhabu ya waovu.
Only with thine eyes shalt thou behold, and see the reward of the wicked.
9 Kama ukimfanya Aliye Juu Sana kuwa makao yako: naam, Bwana ambaye ni kimbilio langu,
Because thou hast made Jehovah, my refuge, the Most High, thy dwelling-place,
10 basi hakuna madhara yatakayokupata wewe, hakuna maafa yataikaribia hema yako.
There shall no evil befall thee, neither shall any plague come nigh thy tent.
11 Kwa kuwa atawaagiza malaika zake kwa ajili yako, wakulinde katika njia zako zote.
For he shall give his angels charge concerning thee, to keep thee in all thy ways:
12 Mikononi mwao watakuinua, ili usijikwae mguu wako kwenye jiwe.
They shall bear thee up in [their] hands, lest thou dash thy foot against a stone.
13 Utawakanyaga simba na nyoka wakali, simba mkubwa na nyoka utawaponda kwa miguu.
Thou shalt tread upon the lion and the adder; the young lion and the dragon shalt thou trample under foot.
14 Bwana asema, “Kwa kuwa ananipenda, nitamwokoa; nitamlinda, kwa kuwa analikiri Jina langu.
Because he hath set his love upon me, therefore will I deliver him; I will set him on high, because he hath known my name.
15 Ataniita, nami nitamjibu; nitakuwa pamoja naye katika taabu, nitamwokoa na kumheshimu.
He shall call upon me, and I will answer him; I will be with him in trouble, I will deliver him and honour him.
16 Kwa siku nyingi nitamshibisha na kumwonyesha wokovu wangu.”
With length of days will I satisfy him, and shew him my salvation.