< Zaburi 90 >

1 Maombi ya Mose, mtu wa Mungu. Bwana, wewe umekuwa makao yetu katika vizazi vyote.
תפלה למשה איש-האלהים אדני--מעון אתה היית לנו בדר ודר
2 Kabla ya kuzaliwa milima au hujaumba dunia na ulimwengu, wewe ni Mungu tangu milele hata milele.
בטרם הרים ילדו-- ותחולל ארץ ותבל ומעולם עד-עולם אתה אל
3 Huwarudisha watu mavumbini, ukisema, “Rudini mavumbini, enyi wanadamu.”
תשב אנוש עד-דכא ותאמר שובו בני-אדם
4 Kwa maana kwako miaka elfu ni kama siku moja iliyokwisha pita, au kama kesha la usiku.
כי אלף שנים בעיניך-- כיום אתמול כי יעבר ואשמורה בלילה
5 Unawatowesha wanadamu katika usingizi wa kifo, nao ni kama majani machanga ya asubuhi:
זרמתם שנה יהיו בבקר כחציר יחלף
6 ingawa asubuhi yanachipua, ifikapo jioni huwa yamenyauka na kukauka.
בבקר יציץ וחלף לערב ימולל ויבש
7 Tumeangamizwa kwa hasira yako na tumetishwa kwa ghadhabu yako.
כי-כלינו באפך ובחמתך נבהלנו
8 Umeyaweka maovu yetu mbele yako, dhambi zetu za siri katika nuru ya uwepo wako.
שת (שתה) עונתינו לנגדך עלמנו למאור פניך
9 Tumeishi siku zetu zote chini ya ghadhabu yako, tunamaliza miaka yetu kwa kuomboleza.
כי כל-ימינו פנו בעברתך כלינו שנינו כמו-הגה
10 Siku zetu za kuishi ni miaka sabini, au miaka themanini ikiwa tuna nguvu, lakini yote ni ya shida na taabu, nazo zapita haraka, nasi twatoweka.
ימי-שנותינו בהם שבעים שנה ואם בגבורת שמונים שנה-- ורהבם עמל ואון כי-גז חיש ונעפה
11 Ni nani ajuaye nguvu za hasira yako? Kwa maana ghadhabu yako ni kubwa kama hofu tunayopaswa kuwa nayo kwako.
מי-יודע עז אפך וכיראתך עברתך
12 Tufundishe kuzihesabu siku zetu vizuri, ili tujipatie moyo wa hekima.
למנות ימינו כן הודע ונבא לבב חכמה
13 Ee Bwana, uwe na huruma! Utakawia hata lini? Wahurumie watumishi wako.
שובה יהוה עד-מתי והנחם על-עבדיך
14 Tushibishe asubuhi kwa upendo wako usiokoma, ili tuweze kuimba kwa shangwe na kufurahi siku zetu zote.
שבענו בבקר חסדך ונרננה ונשמחה בכל-ימינו
15 Utufurahishe kulingana na siku ulizotuadhibu, kulingana na miaka tuliyotaabika.
שמחנו כימות עניתנו שנות ראינו רעה
16 Matendo yako na yaonekane kwa watumishi wako, utukufu wako kwa watoto wao.
יראה אל-עבדיך פעלך והדרך על-בניהם
17 Wema wa Bwana Mungu wetu uwe juu yetu; uzithibitishe kazi za mikono yetu: naam, uzithibitishe kazi za mikono yetu.
ויהי נעם אדני אלהינו-- עלינו ומעשה ידינו כוננה עלינו ומעשה ידינו כוננהו

< Zaburi 90 >