< Zaburi 88 >

1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi leanothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi. Ee Bwana, Mungu uniokoaye, nimelia mbele zako usiku na mchana.
Una canción. Un salmo de los descendientes de Coré. Para el director del coro. Al son de “Mahalath Leannoth”. Un masquil por Hemán el ezraíta Señor, Dios de mi salvación, clamo a ti de día y de noche.
2 Maombi yangu yafike mbele zako, utegee kilio changu sikio lako.
Por favor escucha mi oración; escucha mis palabras de súplica.
3 Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu, na maisha yangu yanakaribia kaburi. (Sheol h7585)
Mi vida está llena de problemas, y mi muerte se acerca. (Sheol h7585)
4 Nimehesabiwa miongoni mwa wale waendao shimoni, niko kama mtu asiye na nguvu.
Soy contado entre los moribundos; un hombre sin fuerzas.
5 Nimetengwa pamoja na wafu, kama waliochinjwa walalao kaburini, ambao huwakumbuki tena, ambao wamekatiliwa mbali na uangalizi wako.
Soy abandonado entre los muertos, tendido como un cadáver en la tumba, olvidado y dejado a tu cuidado.
6 Umenitupa katika shimo lenye kina kirefu sana, katika vina vya giza nene.
Me has puesto en un pozo profundo, entre las penumbras.
7 Ghadhabu yako imekuwa nzito juu yangu, umenigharikisha kwa mawimbi yako yote.
Tu hostilidad me maltrata; me estás ahogando entre tus olas abrumadoras. (Selah)
8 Umenitenga na rafiki zangu wa karibu na kunifanya chukizo kwao. Nimezuiliwa, wala siwezi kutoroka;
Has hecho que mis enemigos me eviten, haciéndome repulsivo a sus vistas. Estoy atrapado, no puedo huir.
9 nuru ya macho yangu imefifia kwa ajili ya huzuni. Ee Bwana, ninakuita kila siku, ninakunyooshea wewe mikono yangu.
Señor, he llorado suplicándote cada día por ayuda, extendiendo mis manos hacia ti.
10 Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako? Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?
¿Haces milagros entre los muertos? ¿Se levantan los muertos para alabarte? (Selah)
11 Je, upendo wako hutangazwa kaburini, uaminifu wako katika Uharibifu?
Tu gran amor, ¿Se menciona en la tumba? Tu fidelidad, ¿Es discutida en lugar de destrucción?
12 Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza, au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?
¿Las cosas maravillosas que haces son conocidas en las tinieblas? ¿Tu bondad es conocida en la tierra del olvido?
13 Lakini ninakulilia wewe, Ee Bwana, unisaidie; asubuhi maombi yangu huja mbele zako.
Pero clamo a ti pidiendo ayuda; cada mañana oro a ti.
14 Ee Bwana, kwa nini unanikataa na kunificha uso wako?
Señor, ¿Por qué me rechazas? ¿Por qué te alejas de mí?
15 Tangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo; nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.
He estado enfermo desde que era joven, a menudo estuve a las puertas de la muerte. He tenido que soportar las cosas terribles que me has hecho. ¡Estoy desesperado!
16 Ghadhabu yako imepita juu yangu; hofu zako zimeniangamiza.
Tu ira me ha vencido; las cosas terribles que haces me han destruido.
17 Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko; zimenimeza kabisa.
Ellos me rodean constantemente como aguas de una inundación, succionándome.
18 Umeniondolea marafiki na wapendwa wangu; giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.
Has hecho que mi familia y mis amigos se alejen. La oscuridad es mi única amiga.

< Zaburi 88 >