< Zaburi 88 >
1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi leanothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi. Ee Bwana, Mungu uniokoaye, nimelia mbele zako usiku na mchana.
Ein Psalmlied. Von den Kindern Korahs. Dem Vorsänger. Auf der Machalat-Leannot. Eine Unterweisung Hemans, des Esrachiten. o HERR, Gott meines Heils, ich schreie Tag und Nacht vor dir!
2 Maombi yangu yafike mbele zako, utegee kilio changu sikio lako.
Laß mein Gebet vor dich kommen, neige dein Ohr zu meinem Flehen;
3 Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu, na maisha yangu yanakaribia kaburi. (Sheol )
denn meine Seele ist der Leiden satt, und mein Lebenslauf neigt sich dem Totenreiche zu. (Sheol )
4 Nimehesabiwa miongoni mwa wale waendao shimoni, niko kama mtu asiye na nguvu.
Ich werde schon zu denen gerechnet, die ins Grab sinken, bin geworden wie ein kraftloser Mann.
5 Nimetengwa pamoja na wafu, kama waliochinjwa walalao kaburini, ambao huwakumbuki tena, ambao wamekatiliwa mbali na uangalizi wako.
Ich liege unter den Toten, bin den Erschlagenen gleich, die im Grabe ruhen, deren du nicht mehr gedenkst und die von deiner Hand abgeschnitten sind.
6 Umenitupa katika shimo lenye kina kirefu sana, katika vina vya giza nene.
Du hast mich in die unterste Grube gelegt, in die Finsternis, in die Tiefe.
7 Ghadhabu yako imekuwa nzito juu yangu, umenigharikisha kwa mawimbi yako yote.
Auf mir lastet dein Grimm, und du bedrängst mich mit allen deinen Wogen. (Pause)
8 Umenitenga na rafiki zangu wa karibu na kunifanya chukizo kwao. Nimezuiliwa, wala siwezi kutoroka;
Du hast alle meine Bekannten von mir entfernt, hast mich ihnen zum Abscheu gemacht; ich bin eingeschlossen und kann nicht heraus.
9 nuru ya macho yangu imefifia kwa ajili ya huzuni. Ee Bwana, ninakuita kila siku, ninakunyooshea wewe mikono yangu.
Mein Auge ist verschmachtet vor Elend; ich habe dich, HERR, täglich angerufen, meine Hände nach dir ausgestreckt.
10 Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako? Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?
Wirst du an den Toten Wunder tun, oder werden die Schatten auferstehen und dich preisen? (Pause)
11 Je, upendo wako hutangazwa kaburini, uaminifu wako katika Uharibifu?
Wird man im Grabe deine Gnade verkündigen, deine Wahrheit im Abgrund?
12 Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza, au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?
Werden deine Wunder in der Finsternis bekanntgemacht, deine Gerechtigkeit im Lande der Vergessenheit?
13 Lakini ninakulilia wewe, Ee Bwana, unisaidie; asubuhi maombi yangu huja mbele zako.
Und doch habe ich zu dir, HERR, geschrieen, und am Morgen kommt dir mein Gebet entgegen.
14 Ee Bwana, kwa nini unanikataa na kunificha uso wako?
Warum, HERR, verwirfst du denn meine Seele und verbirgst dein Angesicht vor mir?
15 Tangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo; nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.
Von Jugend auf bin ich elend und siech, trage deine Schrecken und weiß mir keinen Rat.
16 Ghadhabu yako imepita juu yangu; hofu zako zimeniangamiza.
Deine Zorngerichte sind über mich ergangen, deine Schrecknisse haben mich gänzlich vernichtet.
17 Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko; zimenimeza kabisa.
Sie umgaben mich wie Wasser den ganzen Tag, sie umringten mich allzumal.
18 Umeniondolea marafiki na wapendwa wangu; giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.
Du hast Freunde und Gefährten von mir getan; meine Bekannten sind Finsternis.