< Zaburi 88 >
1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi leanothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi. Ee Bwana, Mungu uniokoaye, nimelia mbele zako usiku na mchana.
Ein Lied. Ein Psalm, der Korachiten. Dem Musikmeister, nach “Krankheit”, zum Singen. Ein Maskil Hemans, des Esrachiten. Jahwe, mein Gott, tagsüber rufe ich um Hilfe, in der Nacht schreie ich vor dir.
2 Maombi yangu yafike mbele zako, utegee kilio changu sikio lako.
Laß mein Gebet vor dich kommen, neige meinem Flehen dein Ohr!
3 Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu, na maisha yangu yanakaribia kaburi. (Sheol )
Denn meine Seele ist mit Leiden gesättigt, und mein Leben ist der Unterwelt nahe. (Sheol )
4 Nimehesabiwa miongoni mwa wale waendao shimoni, niko kama mtu asiye na nguvu.
Ich werde denen zugezählt, die in die Grube hinabfuhren; ich gleiche einem kraftlosen Manne.
5 Nimetengwa pamoja na wafu, kama waliochinjwa walalao kaburini, ambao huwakumbuki tena, ambao wamekatiliwa mbali na uangalizi wako.
Unter die Toten werde ich gerechnet, gleich Erschlagenen, die im Grabe liegen, deren du nicht mehr gedenkst, indem sie von deiner Hand geschieden sind.
6 Umenitupa katika shimo lenye kina kirefu sana, katika vina vya giza nene.
Du hast mich in die unterste Grube gelegt, in dichte Finsternis, in große Tiefe.
7 Ghadhabu yako imekuwa nzito juu yangu, umenigharikisha kwa mawimbi yako yote.
Auf mir lastet dein Grimm, und alle deine Wogen drücken mich nieder. (Sela)
8 Umenitenga na rafiki zangu wa karibu na kunifanya chukizo kwao. Nimezuiliwa, wala siwezi kutoroka;
Du hast meine Bekannten von mir entfernt, hast mich zum Abscheu für sie gemacht; ich bin eingeschlossen und kann nicht hinauskommen.
9 nuru ya macho yangu imefifia kwa ajili ya huzuni. Ee Bwana, ninakuita kila siku, ninakunyooshea wewe mikono yangu.
Mein Auge verschmachtet vor Elend; ich rufe dich, Jahwe, an jedem Tage, ich breite meine Hände zu dir aus.
10 Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako? Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?
Wirst du an den Toten Wunder thun, oder werden die Schatten auferstehen, um dich zu preisen? (Sela)
11 Je, upendo wako hutangazwa kaburini, uaminifu wako katika Uharibifu?
Wird deine Gnade im Grabe verkündigt, deine Treue im Abgrund?
12 Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza, au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?
Werden deine Wunder in der Finsternis kund und deine Gerechtigkeit im Lande des Vergessens?
13 Lakini ninakulilia wewe, Ee Bwana, unisaidie; asubuhi maombi yangu huja mbele zako.
Ich aber schreie zu dir, Jahwe, und mein Gebet kommt des Morgens vor dich.
14 Ee Bwana, kwa nini unanikataa na kunificha uso wako?
Warum verwirfst du, Jahwe, meine Seele, verbirgst vor mir dein Angesicht?
15 Tangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo; nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.
Ich bin elend und hinsterbend von Jugend auf; ich trage deine Schrecken, ich ermatte.
16 Ghadhabu yako imepita juu yangu; hofu zako zimeniangamiza.
Deine Gluten sind über mich ergangen, deine Schrecken haben mich vernichtet.
17 Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko; zimenimeza kabisa.
Sie umgeben mich allezeit wie Wasser, umringen mich insgesamt.
18 Umeniondolea marafiki na wapendwa wangu; giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.
Freunde und Gefährten hast du von mir entfernt; meine Bekannten sind Finsternis.