< Zaburi 88 >

1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi leanothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi. Ee Bwana, Mungu uniokoaye, nimelia mbele zako usiku na mchana.
A Song, a Psalm, by sons of Korah, to the Overseer, 'Concerning the Sickness of Afflictions.' — An instruction, by Heman the Ezrahite. O Jehovah, God of my salvation, Daily I have cried, nightly before Thee,
2 Maombi yangu yafike mbele zako, utegee kilio changu sikio lako.
My prayer cometh in before Thee, Incline Thine ear to my loud cry,
3 Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu, na maisha yangu yanakaribia kaburi. (Sheol h7585)
For my soul hath been full of evils, And my life hath come to Sheol. (Sheol h7585)
4 Nimehesabiwa miongoni mwa wale waendao shimoni, niko kama mtu asiye na nguvu.
I have been reckoned with those going down [to] the pit, I have been as a man without strength.
5 Nimetengwa pamoja na wafu, kama waliochinjwa walalao kaburini, ambao huwakumbuki tena, ambao wamekatiliwa mbali na uangalizi wako.
Among the dead — free, As pierced ones lying in the grave, Whom Thou hast not remembered any more, Yea, they by Thy hand have been cut off.
6 Umenitupa katika shimo lenye kina kirefu sana, katika vina vya giza nene.
Thou hast put me in the lowest pit, In dark places, in depths.
7 Ghadhabu yako imekuwa nzito juu yangu, umenigharikisha kwa mawimbi yako yote.
Upon me hath Thy fury lain, And [with] all Thy breakers Thou hast afflicted. (Selah)
8 Umenitenga na rafiki zangu wa karibu na kunifanya chukizo kwao. Nimezuiliwa, wala siwezi kutoroka;
Thou hast put mine acquaintance far from me, Thou hast made me an abomination to them, Shut up — I go not forth.
9 nuru ya macho yangu imefifia kwa ajili ya huzuni. Ee Bwana, ninakuita kila siku, ninakunyooshea wewe mikono yangu.
Mine eye hath grieved because of affliction, I called Thee, O Jehovah, all the day, I have spread out unto Thee my hands.
10 Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako? Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?
To the dead dost Thou do wonders? Do Rephaim rise? do they thank Thee? (Selah)
11 Je, upendo wako hutangazwa kaburini, uaminifu wako katika Uharibifu?
Is Thy kindness recounted in the grave? Thy faithfulness in destruction?
12 Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza, au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?
Are Thy wonders known in the darkness? And Thy righteousness in the land of forgetfulness?
13 Lakini ninakulilia wewe, Ee Bwana, unisaidie; asubuhi maombi yangu huja mbele zako.
And I, unto Thee, O Jehovah, I have cried, And in the morning doth my prayer come before Thee.
14 Ee Bwana, kwa nini unanikataa na kunificha uso wako?
Why, O Jehovah, castest Thou off my soul? Thou hidest Thy face from me.
15 Tangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo; nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.
I [am] afflicted, and expiring from youth, I have borne Thy terrors — I pine away.
16 Ghadhabu yako imepita juu yangu; hofu zako zimeniangamiza.
Over me hath Thy wrath passed, Thy terrors have cut me off,
17 Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko; zimenimeza kabisa.
They have surrounded me as waters all the day, They have gone round against me together,
18 Umeniondolea marafiki na wapendwa wangu; giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.
Thou hast put far from me lover and friend, Mine acquaintance [is] the place of darkness!

< Zaburi 88 >