< Zaburi 88 >

1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi leanothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi. Ee Bwana, Mungu uniokoaye, nimelia mbele zako usiku na mchana.
Yahweh God, you who rescues me, all during each day I call out [to you] to help me, and I cry out to you during each night also.
2 Maombi yangu yafike mbele zako, utegee kilio changu sikio lako.
Listen [IDM] to my prayer [DOU], while I cry out to you [for help]!
3 Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu, na maisha yangu yanakaribia kaburi. (Sheol h7585)
I have experienced many troubles/difficulties, and I am about to die [MTY] and go where dead people are. (Sheol h7585)
4 Nimehesabiwa miongoni mwa wale waendao shimoni, niko kama mtu asiye na nguvu.
Because I have no more strength, [other people also] consider that I will soon die.
5 Nimetengwa pamoja na wafu, kama waliochinjwa walalao kaburini, ambao huwakumbuki tena, ambao wamekatiliwa mbali na uangalizi wako.
I am like a corpse that has been abandoned; I am like dead people who lie in their graves, people who have been completely forgotten, because you do not take care of them any more.
6 Umenitupa katika shimo lenye kina kirefu sana, katika vina vya giza nene.
[It is as though] you have thrown me into a deep, dark pit, into a place where they throw corpses.
7 Ghadhabu yako imekuwa nzito juu yangu, umenigharikisha kwa mawimbi yako yote.
[It seems like] you are very angry with me, and [it is as though] you have crushed me like [ocean] waves [crash down on people] [MET].
8 Umenitenga na rafiki zangu wa karibu na kunifanya chukizo kwao. Nimezuiliwa, wala siwezi kutoroka;
You have caused my friends to (avoid/stay away from) me; I have become repulsive to them. [It is as though] I am in a prison and cannot escape.
9 nuru ya macho yangu imefifia kwa ajili ya huzuni. Ee Bwana, ninakuita kila siku, ninakunyooshea wewe mikono yangu.
My eyes cannot see well because I cry very much. Yahweh, every day I call out to you [to help me]; I lift up my hands to you [while I pray].
10 Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako? Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?
You certainly do not [RHQ] perform miracles for dead people! Their spirits do not [RHQ] arise to praise you!
11 Je, upendo wako hutangazwa kaburini, uaminifu wako katika Uharibifu?
Corpses in the grave certainly do not tell about your faithfully loving us [RHQ], and in the place where people are finally destroyed, no one tells about what you faithfully [do for us] [RHQ].
12 Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza, au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?
No one in the deep dark pit ever sees the miracles that you perform [RHQ], and no one in the place where people have been completely forgotten tells about your being good to us.
13 Lakini ninakulilia wewe, Ee Bwana, unisaidie; asubuhi maombi yangu huja mbele zako.
But [as for me], Yahweh, I cry out to you [to help me]; each morning I pray to you.
14 Ee Bwana, kwa nini unanikataa na kunificha uso wako?
Yahweh, why do you reject me [RHQ]? Why do you turn away from me [RHQ]?
15 Tangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo; nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.
All the time since I was young, I have suffered and have often almost died; I am (in despair/very discouraged) because of enduring the terrible things that you have done to me.
16 Ghadhabu yako imepita juu yangu; hofu zako zimeniangamiza.
[I feel that] you have crushed me because of your being angry with me; the terrible things that you are doing to me are almost destroying me.
17 Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko; zimenimeza kabisa.
[I feel as though] they surround me like a flood [SIM]; they are (closing in on/crushing) me from all sides.
18 Umeniondolea marafiki na wapendwa wangu; giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.
You have caused [even] my friends and others whom I love to avoid me, and [it is as though] the only friend that I have is darkness.

< Zaburi 88 >