< Zaburi 88 >

1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi leanothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi. Ee Bwana, Mungu uniokoaye, nimelia mbele zako usiku na mchana.
A Song, a psalm of the Korahites. To the leader: according to Mahalath Leannoth. A Maskil of Heman the Ezrahite. O Lord my God, I cry for help in the day-time, in the night my cry is before you;
2 Maombi yangu yafike mbele zako, utegee kilio changu sikio lako.
let my prayer come into your presence, incline your ear to my cry.
3 Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu, na maisha yangu yanakaribia kaburi. (Sheol h7585)
For I am sated with sorrow, my life draws near to Sheol. (Sheol h7585)
4 Nimehesabiwa miongoni mwa wale waendao shimoni, niko kama mtu asiye na nguvu.
I am counted with those who go down to the pit; without strength am I.
5 Nimetengwa pamoja na wafu, kama waliochinjwa walalao kaburini, ambao huwakumbuki tena, ambao wamekatiliwa mbali na uangalizi wako.
My home is among the dead, like the slain that lie in the grave, whom you remember no more cut off as they are from your hand.
6 Umenitupa katika shimo lenye kina kirefu sana, katika vina vya giza nene.
In the deepest pit you have put me, in shadows deep and dark.
7 Ghadhabu yako imekuwa nzito juu yangu, umenigharikisha kwa mawimbi yako yote.
Your wrath lies heavy upon me, waves of your anger roll over me. (Selah)
8 Umenitenga na rafiki zangu wa karibu na kunifanya chukizo kwao. Nimezuiliwa, wala siwezi kutoroka;
You have put my friends far from me, you have made them shun me. I am shut in, and cannot escape,
9 nuru ya macho yangu imefifia kwa ajili ya huzuni. Ee Bwana, ninakuita kila siku, ninakunyooshea wewe mikono yangu.
my eyes are wasted with sorrow. I call on you, Lord, every day, spreading my hands out to you.
10 Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako? Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?
For the dead can you work wonders? Can the shades rise again to praise you? (Selah)
11 Je, upendo wako hutangazwa kaburini, uaminifu wako katika Uharibifu?
Can your kindness be told in the grave, your faithfulness in the tomb?
12 Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza, au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?
Can your wonders be known in the darkness, or your help in the land of forgetfulness?
13 Lakini ninakulilia wewe, Ee Bwana, unisaidie; asubuhi maombi yangu huja mbele zako.
I cry for help to you, in the morning my prayer comes before you.
14 Ee Bwana, kwa nini unanikataa na kunificha uso wako?
Why, O Lord, do you spurn me, and hide your face from me?
15 Tangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo; nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.
From my youth I am wretched and dying, I am numbed by the terrors I bear.
16 Ghadhabu yako imepita juu yangu; hofu zako zimeniangamiza.
The fires of your wrath have passed over me, your terrors destroy me,
17 Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko; zimenimeza kabisa.
surging around me forever, hemming me in altogether.
18 Umeniondolea marafiki na wapendwa wangu; giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.
Those who love me you put far from me; the dark is my only friend.

< Zaburi 88 >