< Zaburi 88 >
1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi leanothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi. Ee Bwana, Mungu uniokoaye, nimelia mbele zako usiku na mchana.
“A psalm of the sons of Korah. For the leader of the music. Upon wind instruments. A psalm of Heman, the Ezrahite.” O LORD, God of my salvation! To thee do I cry by day, And by night is my prayer before thee!
2 Maombi yangu yafike mbele zako, utegee kilio changu sikio lako.
Let my supplication come before thee; Incline thine ear to my cry!
3 Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu, na maisha yangu yanakaribia kaburi. (Sheol )
For my soul is full of misery, And my life draweth near to the underworld. (Sheol )
4 Nimehesabiwa miongoni mwa wale waendao shimoni, niko kama mtu asiye na nguvu.
I am counted with those who are going down to the pit; I am like one who hath no strength.
5 Nimetengwa pamoja na wafu, kama waliochinjwa walalao kaburini, ambao huwakumbuki tena, ambao wamekatiliwa mbali na uangalizi wako.
I am left to myself among the dead, Like the slain who lie in the grave, Whom thou no more rememberest, And who are cut off from thy [[protecting]] hand.
6 Umenitupa katika shimo lenye kina kirefu sana, katika vina vya giza nene.
Thou hast placed me in a deep pit, In a dark and deep abyss.
7 Ghadhabu yako imekuwa nzito juu yangu, umenigharikisha kwa mawimbi yako yote.
Thy wrath presseth hard upon me, And thou afflictest me with all thy waves! (Pause)
8 Umenitenga na rafiki zangu wa karibu na kunifanya chukizo kwao. Nimezuiliwa, wala siwezi kutoroka;
Thou hast put mine acquaintances far from me, Yea, thou hast made me their abhorrence: I am shut up, and cannot go forth.
9 nuru ya macho yangu imefifia kwa ajili ya huzuni. Ee Bwana, ninakuita kila siku, ninakunyooshea wewe mikono yangu.
Mine eyes languish by reason of my affliction. I call upon thee daily, O LORD! To thee do I stretch out my hands!
10 Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako? Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?
Canst thou show wonders to the dead? Shall the dead arise, and praise thee? (Pause)
11 Je, upendo wako hutangazwa kaburini, uaminifu wako katika Uharibifu?
Shall thy goodness be declared in the grave, Or thy faithfulness in the place of corruption?
12 Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza, au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?
Shall thy wonders be known in the dark, And thy justice in the land of forgetfulness?
13 Lakini ninakulilia wewe, Ee Bwana, unisaidie; asubuhi maombi yangu huja mbele zako.
To thee do I cry, O LORD! In the morning doth my cry come before thee.
14 Ee Bwana, kwa nini unanikataa na kunificha uso wako?
Why, O LORD! dost thou cast me off? Why hidest thou thy face from me?
15 Tangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo; nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.
I have been afflicted and languishing from my youth; I suffer thy terrors, and am distracted.
16 Ghadhabu yako imepita juu yangu; hofu zako zimeniangamiza.
Thy fierce wrath overwhelmeth me; Thy terrors utterly destroy me.
17 Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko; zimenimeza kabisa.
They surround me daily like water; They compass me about together.
18 Umeniondolea marafiki na wapendwa wangu; giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.
Lover and friend hast thou put far from me; My acquaintances are withdrawn from my sight.