< Zaburi 88 >
1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi leanothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi. Ee Bwana, Mungu uniokoaye, nimelia mbele zako usiku na mchana.
A SONG. A PSALM OF THE SONS OF KORAH. TO THE OVERSEER. [SET] ON “SICKNESS TO AFFLICT.” AN INSTRUCTION OF HEMAN THE EZRAHITE. O YHWH, God of my salvation, Daily I have cried, nightly before You,
2 Maombi yangu yafike mbele zako, utegee kilio changu sikio lako.
My prayer comes in before You, Incline Your ear to my loud cry,
3 Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu, na maisha yangu yanakaribia kaburi. (Sheol )
For my soul has been full of evils, And my life has come to Sheol. (Sheol )
4 Nimehesabiwa miongoni mwa wale waendao shimoni, niko kama mtu asiye na nguvu.
I have been reckoned with those going down [to] the pit, I have been as a man without strength.
5 Nimetengwa pamoja na wafu, kama waliochinjwa walalao kaburini, ambao huwakumbuki tena, ambao wamekatiliwa mbali na uangalizi wako.
Among the dead—free, As pierced ones lying in the grave, Whom You have not remembered anymore, Indeed, they have been cut off by Your hand.
6 Umenitupa katika shimo lenye kina kirefu sana, katika vina vya giza nene.
You have put me in the lowest pit, In dark places, in depths.
7 Ghadhabu yako imekuwa nzito juu yangu, umenigharikisha kwa mawimbi yako yote.
Your fury has lain on me, And You have afflicted [with] all Your breakers. (Selah)
8 Umenitenga na rafiki zangu wa karibu na kunifanya chukizo kwao. Nimezuiliwa, wala siwezi kutoroka;
You have put my acquaintance far from me, You have made me an abomination to them, Shut up—I do not go forth.
9 nuru ya macho yangu imefifia kwa ajili ya huzuni. Ee Bwana, ninakuita kila siku, ninakunyooshea wewe mikono yangu.
My eye has grieved because of affliction, I called You, O YHWH, all the day, I have spread out my hands to You.
10 Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako? Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?
Do You do wonders to the dead? Does Rephaim rise? Do they thank You? (Selah)
11 Je, upendo wako hutangazwa kaburini, uaminifu wako katika Uharibifu?
Is Your kindness recounted in the grave? Your faithfulness in destruction?
12 Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza, au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?
Are Your wonders known in the darkness? And Your righteousness in the land of forgetfulness?
13 Lakini ninakulilia wewe, Ee Bwana, unisaidie; asubuhi maombi yangu huja mbele zako.
And I, to You, O YHWH, I have cried, And in the morning my prayer comes before You.
14 Ee Bwana, kwa nini unanikataa na kunificha uso wako?
Why, O YHWH, do You cast off my soul? You hide Your face from me.
15 Tangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo; nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.
I [am] afflicted, and expiring from youth, I have borne Your terrors—I pine away.
16 Ghadhabu yako imepita juu yangu; hofu zako zimeniangamiza.
Your wrath has passed over me, Your terrors have cut me off,
17 Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko; zimenimeza kabisa.
They have surrounded me as waters all the day, They have gone around against me together,
18 Umeniondolea marafiki na wapendwa wangu; giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.
You have put lover and friend far from me, My acquaintance [is] the place of darkness!