< Zaburi 88 >
1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi leanothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi. Ee Bwana, Mungu uniokoaye, nimelia mbele zako usiku na mchana.
“A song or psalm of the sons of Korach, to the chief musician upon Machalath-le'annoth, a Maskil of Heman the Ezrachite.” O Lord the God of my salvation, by day do I cry, [and] at night I am before thee.
2 Maombi yangu yafike mbele zako, utegee kilio changu sikio lako.
Let my prayer come unto thy presence; incline thy ear unto my entreaty.
3 Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu, na maisha yangu yanakaribia kaburi. (Sheol )
For my soul is sated with troubles; and my life draweth nigh unto the nether world. (Sheol )
4 Nimehesabiwa miongoni mwa wale waendao shimoni, niko kama mtu asiye na nguvu.
I am counted with those that descend into the pit; I am become as a man without vigor:
5 Nimetengwa pamoja na wafu, kama waliochinjwa walalao kaburini, ambao huwakumbuki tena, ambao wamekatiliwa mbali na uangalizi wako.
Free among the dead, like the slain that dwell in the grave, whom thou rememberest no more; and those that are cut off by thy hand.
6 Umenitupa katika shimo lenye kina kirefu sana, katika vina vya giza nene.
Thou hast laid me in the pit of the lower world, in darkness, in the depths.
7 Ghadhabu yako imekuwa nzito juu yangu, umenigharikisha kwa mawimbi yako yote.
Upon me lieth heavily thy fury, and with all thy billows hast thou afflicted me. (Selah)
8 Umenitenga na rafiki zangu wa karibu na kunifanya chukizo kwao. Nimezuiliwa, wala siwezi kutoroka;
Thou hast removed my acquaintances far from me; thou hast rendered me an abomination unto them: I am imprisoned, and I cannot go forth.
9 nuru ya macho yangu imefifia kwa ajili ya huzuni. Ee Bwana, ninakuita kila siku, ninakunyooshea wewe mikono yangu.
My eye languisheth by reason of affliction: I call on thee, O Lord, every day, I stretch out unto thee my hands.
10 Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako? Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?
Wilt thou display wonders to the dead? shall the departed arise [and] thank thee? (Selah)
11 Je, upendo wako hutangazwa kaburini, uaminifu wako katika Uharibifu?
Shall thy kindness be related in the grave? thy faithfulness in the place of corruption?
12 Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza, au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?
Shall thy wonders be acknowledged in the darkness? and thy righteousness in the land of forgetfulness?
13 Lakini ninakulilia wewe, Ee Bwana, unisaidie; asubuhi maombi yangu huja mbele zako.
Yet I cry indeed aloud unto thee, O Lord; and in the morning shall my prayer come before thee.
14 Ee Bwana, kwa nini unanikataa na kunificha uso wako?
Why, O Lord, wilt thou cast off my soul? [why] wilt thou hide thy face from me?
15 Tangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo; nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.
I am afflicted and perishing from my youth up: I bear thy terrors, I am distracted.
16 Ghadhabu yako imepita juu yangu; hofu zako zimeniangamiza.
Over me have the fires of thy wrath passed; thy terrors have destroyed me;
17 Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko; zimenimeza kabisa.
They encompass me like water all the time; they have closed in round about me together.
18 Umeniondolea marafiki na wapendwa wangu; giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.
Thou hast removed far from me lover and friend, my acquaintances [are in] darkness.