< Zaburi 88 >

1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi leanothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi. Ee Bwana, Mungu uniokoaye, nimelia mbele zako usiku na mchana.
A song or Psalme of Heman the Ezrahite to give instruction, committed to the sonnes of Korah for him that excelleth upon Malath Leannoth. O Lord God of my saluation, I cry day and night before thee.
2 Maombi yangu yafike mbele zako, utegee kilio changu sikio lako.
Let my prayer enter into thy presence: incline thine eare vnto my cry.
3 Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu, na maisha yangu yanakaribia kaburi. (Sheol h7585)
For my soule is filled with euils, and my life draweth neere to the graue. (Sheol h7585)
4 Nimehesabiwa miongoni mwa wale waendao shimoni, niko kama mtu asiye na nguvu.
I am counted among them that go downe vnto the pit, and am as a man without strength:
5 Nimetengwa pamoja na wafu, kama waliochinjwa walalao kaburini, ambao huwakumbuki tena, ambao wamekatiliwa mbali na uangalizi wako.
Free among the dead, like the slaine lying in the graue, whome thou remembrest no more, and they are cut off from thine hand.
6 Umenitupa katika shimo lenye kina kirefu sana, katika vina vya giza nene.
Thou hast layde me in the lowest pit, in darkenes, and in the deepe.
7 Ghadhabu yako imekuwa nzito juu yangu, umenigharikisha kwa mawimbi yako yote.
Thine indignation lyeth vpon me, and thou hast vexed me with all thy waues. (Selah)
8 Umenitenga na rafiki zangu wa karibu na kunifanya chukizo kwao. Nimezuiliwa, wala siwezi kutoroka;
Thou hast put away mine acquaintance farre from me, and made mee to be abhorred of them: I am shut vp, and cannot get foorth.
9 nuru ya macho yangu imefifia kwa ajili ya huzuni. Ee Bwana, ninakuita kila siku, ninakunyooshea wewe mikono yangu.
Mine eye is sorowfull through mine affliction: Lord, I call dayly vpon thee: I stretch out mine hands vnto thee.
10 Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako? Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?
Wilt thou shewe a miracle to the dead? or shall the dead rise and prayse thee? (Selah)
11 Je, upendo wako hutangazwa kaburini, uaminifu wako katika Uharibifu?
Shall thy louing kindenes be declared in the graue? or thy faithfulnes in destruction?
12 Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza, au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?
Shall thy wonderous workes be knowen in the darke? and thy righteousnes in the land of obliuion?
13 Lakini ninakulilia wewe, Ee Bwana, unisaidie; asubuhi maombi yangu huja mbele zako.
But vnto thee haue I cryed, O Lord, and early shall my prayer come before thee.
14 Ee Bwana, kwa nini unanikataa na kunificha uso wako?
Lord, why doest thou reiect my soule, and hidest thy face from me?
15 Tangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo; nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.
I am afflicted and at the point of death: from my youth I suffer thy terrours, doubting of my life.
16 Ghadhabu yako imepita juu yangu; hofu zako zimeniangamiza.
Thine indignations goe ouer me, and thy feare hath cut me off.
17 Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko; zimenimeza kabisa.
They came round about me dayly like water, and compassed me together.
18 Umeniondolea marafiki na wapendwa wangu; giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.
My louers and friends hast thou put away from me, and mine acquaintance hid themselues.

< Zaburi 88 >