< Zaburi 88 >
1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi leanothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi. Ee Bwana, Mungu uniokoaye, nimelia mbele zako usiku na mchana.
A Song. A Psalm. Of the sons of Korah. To the chief music-maker; put to Mahalath Leannoth. Maschil. Of Heman the Ezrahite. O Lord, God of my salvation, I have been crying to you for help by day and by night:
2 Maombi yangu yafike mbele zako, utegee kilio changu sikio lako.
Let my prayer come before you; give ear to my cry:
3 Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu, na maisha yangu yanakaribia kaburi. (Sheol )
For my soul is full of evils, and my life has come near to the underworld. (Sheol )
4 Nimehesabiwa miongoni mwa wale waendao shimoni, niko kama mtu asiye na nguvu.
I am numbered among those who go down into the earth; I have become like a man for whom there is no help:
5 Nimetengwa pamoja na wafu, kama waliochinjwa walalao kaburini, ambao huwakumbuki tena, ambao wamekatiliwa mbali na uangalizi wako.
My soul is among the dead, like those in the underworld, to whom you give no more thought; for they are cut off from your care.
6 Umenitupa katika shimo lenye kina kirefu sana, katika vina vya giza nene.
You have put me in the lowest deep, even in dark places.
7 Ghadhabu yako imekuwa nzito juu yangu, umenigharikisha kwa mawimbi yako yote.
The weight of your wrath is crushing me, all your waves have overcome me. (Selah)
8 Umenitenga na rafiki zangu wa karibu na kunifanya chukizo kwao. Nimezuiliwa, wala siwezi kutoroka;
You have sent my friends far away from me; you have made me a disgusting thing in their eyes: I am shut up, and not able to come out.
9 nuru ya macho yangu imefifia kwa ajili ya huzuni. Ee Bwana, ninakuita kila siku, ninakunyooshea wewe mikono yangu.
My eyes are wasting away because of my trouble: Lord, my cry has gone up to you every day, my hands are stretched out to you.
10 Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako? Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?
Will you do works of wonder for the dead? will the shades come back to give you praise? (Selah)
11 Je, upendo wako hutangazwa kaburini, uaminifu wako katika Uharibifu?
Will the story of your mercy be given in the house of the dead? will news of your faith come to the place of destruction?
12 Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza, au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?
May there be knowledge of your wonders in the dark? or of your righteousness where memory is dead?
13 Lakini ninakulilia wewe, Ee Bwana, unisaidie; asubuhi maombi yangu huja mbele zako.
But to you did I send up my cry, O Lord; in the morning my prayer came before you.
14 Ee Bwana, kwa nini unanikataa na kunificha uso wako?
Lord, why have you sent away my soul? why is your face covered from me?
15 Tangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo; nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.
I have been troubled and in fear of death from the time when I was young; your wrath is hard on me, and I have no strength.
16 Ghadhabu yako imepita juu yangu; hofu zako zimeniangamiza.
The heat of your wrath has gone over me; I am broken by your cruel punishments.
17 Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko; zimenimeza kabisa.
They are round me all the day like water; they have made a circle about me.
18 Umeniondolea marafiki na wapendwa wangu; giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.
You have sent my friends and lovers far from me; I am gone from the memory of those who are dear to me.