< Zaburi 87 >

1 Zaburi ya wana wa Kora. Wimbo. Ameuweka msingi wake katika mlima mtakatifu;
Salmo di Cantico de' figliuoli di Core LA fondazione del Signore[è] ne' monti santi.
2 Bwana anayapenda malango ya Sayuni kuliko makao yote ya Yakobo.
Il Signore ama le porte di Sion, Sopra tutte le stanze di Giacobbe.
3 Mambo matukufu yanasemwa juu yako, ee mji wa Mungu:
O Città di Dio, Cose gloriose son dette di te. (Sela)
4 “Nitaweka kumbukumbu ya Rahabu na Babeli miongoni mwa wale wanaonikubali mimi: Ufilisti pia na Tiro, pamoja na Kushi, nami nitasema, ‘Huyu alizaliwa Sayuni.’”
Io mentoverò, [dice al Signore], Rahab, e Babilonia, Fra quelli che mi conoscono; Ecco, i Filistei ed i Tiri insieme con gli Etiopi, [De' quali si dirà: ] Costui è nato quivi.
5 Kuhusu Sayuni itasemwa hivi, “Huyu na yule walizaliwa humo, naye Aliye Juu Sana mwenyewe atamwimarisha.”
E si dirà di Sion: Questi e quegli è nato in essa; E l'Altissimo stesso la stabilirà.
6 Bwana ataandika katika orodha ya mataifa: “Huyu alizaliwa Sayuni.”
Il Signore, rassegnando i popoli, annovererà [coloro], [Dicendo: ] Un tale è nato quivi. (Sela)
7 Watakapokuwa wanapiga vinanda wataimba, “Chemchemi zangu zote ziko kwako.”
E cantori, e suonatori, E tutte le mie fonti, [saranno] in te.

< Zaburi 87 >