< Zaburi 87 >
1 Zaburi ya wana wa Kora. Wimbo. Ameuweka msingi wake katika mlima mtakatifu;
Von den Korahiten ein Psalm, ein Lied.
2 Bwana anayapenda malango ya Sayuni kuliko makao yote ya Yakobo.
lieb hat der HERR die Tore Zions mehr als alle (anderen) Wohnstätten Jakobs.
3 Mambo matukufu yanasemwa juu yako, ee mji wa Mungu:
Herrliches ist von dir berichtet, du Gottesstadt. (SELA)
4 “Nitaweka kumbukumbu ya Rahabu na Babeli miongoni mwa wale wanaonikubali mimi: Ufilisti pia na Tiro, pamoja na Kushi, nami nitasema, ‘Huyu alizaliwa Sayuni.’”
»Ich nenne Ägypten und Babel als meine Bekenner, hier das Philisterland und Tyrus samt Äthiopien – nämlich wer dort seine Heimat hat.«
5 Kuhusu Sayuni itasemwa hivi, “Huyu na yule walizaliwa humo, naye Aliye Juu Sana mwenyewe atamwimarisha.”
Doch von Zion heißt es: »Mann für Mann hat dort seine Heimat, und er selbst, der Höchste, macht es stark.«
6 Bwana ataandika katika orodha ya mataifa: “Huyu alizaliwa Sayuni.”
Der HERR zählt, wenn er die Völker aufschreibt: »Dieser hat dort seine Heimat.« (SELA)
7 Watakapokuwa wanapiga vinanda wataimba, “Chemchemi zangu zote ziko kwako.”
Sie aber tanzen den Reigen und singen: »Alle meine Quellen sind in dir (o Zion)!«