< Zaburi 87 >

1 Zaburi ya wana wa Kora. Wimbo. Ameuweka msingi wake katika mlima mtakatifu;
Von den Korachiten, ein Lied, ein Gesang. - Was er auf heiligen Bergen hat gegründet
2 Bwana anayapenda malango ya Sayuni kuliko makao yote ya Yakobo.
das liebt der Herr; die Sionstore mehr als alle andern Wohnungen Jakobs.
3 Mambo matukufu yanasemwa juu yako, ee mji wa Mungu:
Von dir ist Herrliches zu künden, du Gottesstadt. (Sela)
4 “Nitaweka kumbukumbu ya Rahabu na Babeli miongoni mwa wale wanaonikubali mimi: Ufilisti pia na Tiro, pamoja na Kushi, nami nitasema, ‘Huyu alizaliwa Sayuni.’”
Erwähne ich auch Rahab und auch Babel wegen ihrer Weisen, Philisterland und Tyrus und Äthiopien: "Es ist dort der geboren",
5 Kuhusu Sayuni itasemwa hivi, “Huyu na yule walizaliwa humo, naye Aliye Juu Sana mwenyewe atamwimarisha.”
so wird von Sion ausgesagt: "Darin ist Mann um Mann geboren." Das sichert ihm den höchsten Rang.
6 Bwana ataandika katika orodha ya mataifa: “Huyu alizaliwa Sayuni.”
Der Herr ist's, der bestätigt, zeichnet er die Völker auf: "Es ist der dort geboren." (Sela)
7 Watakapokuwa wanapiga vinanda wataimba, “Chemchemi zangu zote ziko kwako.”
So singt und tanzt, wer immer in dir wohnt.

< Zaburi 87 >