< Zaburi 87 >

1 Zaburi ya wana wa Kora. Wimbo. Ameuweka msingi wake katika mlima mtakatifu;
A Psalm [or] Song for the sons of Korah. His foundation [is] in the holy mountains.
2 Bwana anayapenda malango ya Sayuni kuliko makao yote ya Yakobo.
The LORD loveth the gates of Zion more than all the dwellings of Jacob.
3 Mambo matukufu yanasemwa juu yako, ee mji wa Mungu:
Glorious things are spoken of thee, O city of God. (Selah)
4 “Nitaweka kumbukumbu ya Rahabu na Babeli miongoni mwa wale wanaonikubali mimi: Ufilisti pia na Tiro, pamoja na Kushi, nami nitasema, ‘Huyu alizaliwa Sayuni.’”
I will make mention of Rahab and Babylon to them that know me: behold Philistia, and Tyre, with Cush; this [man] was born there.
5 Kuhusu Sayuni itasemwa hivi, “Huyu na yule walizaliwa humo, naye Aliye Juu Sana mwenyewe atamwimarisha.”
And of Zion it shall be said, This and that man was born in her: and the Highest himself shall establish her.
6 Bwana ataandika katika orodha ya mataifa: “Huyu alizaliwa Sayuni.”
The LORD shall count, when he writeth up the people, [that] this [man] was born there. (Selah)
7 Watakapokuwa wanapiga vinanda wataimba, “Chemchemi zangu zote ziko kwako.”
As well the singers as the players on instruments [shall be there]: all my springs [are] in thee.

< Zaburi 87 >