< Zaburi 87 >

1 Zaburi ya wana wa Kora. Wimbo. Ameuweka msingi wake katika mlima mtakatifu;
Of the Korahites, a psalm. A song. On the holy mountain stands the city he founded.
2 Bwana anayapenda malango ya Sayuni kuliko makao yote ya Yakobo.
The Lord loves the gates of Zion more than all the dwellings of Jacob.
3 Mambo matukufu yanasemwa juu yako, ee mji wa Mungu:
Glorious things he is speaking of you, you city of God. (Selah)
4 “Nitaweka kumbukumbu ya Rahabu na Babeli miongoni mwa wale wanaonikubali mimi: Ufilisti pia na Tiro, pamoja na Kushi, nami nitasema, ‘Huyu alizaliwa Sayuni.’”
“Among those who are mine I name Rahab and Babylon, Philistia, Tyre, Ethiopia, their people will say I was born in Zion.
5 Kuhusu Sayuni itasemwa hivi, “Huyu na yule walizaliwa humo, naye Aliye Juu Sana mwenyewe atamwimarisha.”
As for Zion it will be said each and all were born in her.” The Lord will preserve her.
6 Bwana ataandika katika orodha ya mataifa: “Huyu alizaliwa Sayuni.”
The Lord will count, when enrolling the peoples, “This one was born there, and that one was born there.” (Selah)
7 Watakapokuwa wanapiga vinanda wataimba, “Chemchemi zangu zote ziko kwako.”
Singers and dancers alike will say “All my springs are in you.”

< Zaburi 87 >