< Zaburi 87 >

1 Zaburi ya wana wa Kora. Wimbo. Ameuweka msingi wake katika mlima mtakatifu;
A Psalm of the sons of Korah; a Song. His foundation is in the holy mountains.
2 Bwana anayapenda malango ya Sayuni kuliko makao yote ya Yakobo.
The LORD loveth the gates of Zion more than all the dwellings of Jacob.
3 Mambo matukufu yanasemwa juu yako, ee mji wa Mungu:
Glorious things are spoken of Thee, O city of God. (Selah)
4 “Nitaweka kumbukumbu ya Rahabu na Babeli miongoni mwa wale wanaonikubali mimi: Ufilisti pia na Tiro, pamoja na Kushi, nami nitasema, ‘Huyu alizaliwa Sayuni.’”
'I will make mention of Rahab and Babylon as among them that know Me; behold Philistia, and Tyre, with Ethiopia; this one was born there.'
5 Kuhusu Sayuni itasemwa hivi, “Huyu na yule walizaliwa humo, naye Aliye Juu Sana mwenyewe atamwimarisha.”
But of Zion it shall be said: 'This man and that was born in her; and the Most High Himself doth establish her.'
6 Bwana ataandika katika orodha ya mataifa: “Huyu alizaliwa Sayuni.”
The LORD shall count in the register of the peoples: 'This one was born there.' (Selah)
7 Watakapokuwa wanapiga vinanda wataimba, “Chemchemi zangu zote ziko kwako.”
And whether they sing or dance, all my thoughts are in Thee.

< Zaburi 87 >