< Zaburi 86 >
1 Maombi ya Daudi. Ee Bwana, sikia na unijibu, kwa maana mimi ni maskini na mhitaji.
Abre tus oídos a mi voz, oh Señor, y dame una respuesta; porque estoy afligido y tengo necesidad.
2 Linda maisha yangu, kwa maana nimejiweka kwako, wewe ni Mungu wangu, mwokoe mtumishi wako anayekutumaini.
Guarda mi alma, porque soy fiel a ti; Oh mi Dios, da la salvación a tu siervo, cuya esperanza está en ti.
3 Ee Bwana, nihurumie mimi, kwa maana ninakuita mchana kutwa.
Ten misericordia de mí, oh Señor; porque mi llanto va hasta ti todo el día.
4 Mpe mtumishi wako furaha, kwa kuwa kwako wewe, Ee Bwana, ninainua nafsi yangu.
Alegra el alma de tu siervo; porque está elevada a ti, oh Señor.
5 Ee Bwana, wewe ni mwema na mwenye kusamehe, umejaa upendo kwa wote wakuitao.
Eres bueno, oh Señor, y lleno de perdón; tu misericordia es grandiosa para todos los que te claman.
6 Ee Bwana, sikia maombi yangu, sikiliza kilio changu unihurumie.
Oh Señor, escucha mi oración; atiende a mi plegaria.
7 Katika siku ya shida yangu nitakuita, kwa maana wewe utanijibu.
En el día de mi angustia, te clamo; porque me darás una respuesta.
8 Ee Bwana, katikati ya miungu hakuna kama wewe, hakuna matendo ya kulinganishwa na yako.
No hay dios como tú, oh Señor; no hay obras como tus obras.
9 Ee Bwana, mataifa yote uliyoyafanya yatakuja na kuabudu mbele zako; wataliletea utukufu jina lako.
Vengan todas las naciones tuyas, y adoren, oh Jehová, glorificando tu nombre.
10 Kwa maana wewe ni mkuu, na unafanya mambo ya ajabu; wewe peke yako ndiwe Mungu.
Porque tú eres grande, y haces grandes obras de asombro; solo eres Dios.
11 Ee Bwana, nifundishe njia yako, nami nitakwenda katika kweli yako; nipe moyo usiositasita, ili niweze kulicha jina lako.
Abre tu camino a mí, oh Señor; Seguiré mi camino en tu fe: deja que mi corazón se alegre con el temor de tu nombre.
12 Ee Bwana wangu, nitakusifu kwa moyo wote; nitaliadhimisha jina lako milele.
Te alabaré, oh Jehová Dios mío, de todo corazón; Daré gloria a tu nombre para siempre.
13 Kwa maana upendo wako ni mkuu kwangu; umeniokoa kutoka kwenye vilindi vya kaburi. (Sheol )
Porque tu misericordia conmigo es grande; has sacado mi alma de los lugares profundos del inframundo. (Sheol )
14 Ee Mungu, wenye majivuno wananishambulia; kundi la watu wakatili linatafuta uhai wangu: watu wasiokuheshimu wewe.
Oh Dios, hombres de orgullo se han levantado contra mí, y el ejército de hombres violentos buscan mi vida; no te han puesto delante de ellos.
15 Lakini wewe, Ee Bwana, ni Mungu wa huruma na neema, si mwepesi wa hasira, bali ni mwingi wa upendo na uaminifu.
Pero tú, oh Señor, eres un Dios lleno de compasión y perdón, lento para enojarte, grande en misericordia y verdad.
16 Nigeukie na unihurumie; mpe mtumishi wako nguvu zako, mwokoe mwana wa mtumishi wako wa kike.
Mírame, y ten misericordia de mí! da fortaleza a tu siervo, y tu salvación al hijo de tu sierva.
17 Nipe ishara ya wema wako, ili adui zangu waione nao waaibishwe, kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umenisaidia na kunifariji.
Dame una señal para el bien; para que mis enemigos lo vean y se avergüencen; porque tú, Señor, has sido mi ayuda y mi consuelo.