< Zaburi 86 >

1 Maombi ya Daudi. Ee Bwana, sikia na unijibu, kwa maana mimi ni maskini na mhitaji.
Inclina, Senhor, os teus ouvidos, e ouve-me, porque estou necessitado e aflito.
2 Linda maisha yangu, kwa maana nimejiweka kwako, wewe ni Mungu wangu, mwokoe mtumishi wako anayekutumaini.
Guarda a minha alma, pois sou santo; oh Deus meu, salva o teu servo, que em ti confia.
3 Ee Bwana, nihurumie mimi, kwa maana ninakuita mchana kutwa.
Tem misericórdia de mim, ó Senhor, pois a ti clamo todo o dia.
4 Mpe mtumishi wako furaha, kwa kuwa kwako wewe, Ee Bwana, ninainua nafsi yangu.
Alegra a alma do teu servo, pois a ti, Senhor, levanto a minha alma.
5 Ee Bwana, wewe ni mwema na mwenye kusamehe, umejaa upendo kwa wote wakuitao.
Pois tu, Senhor, és bom, e pronto a perdoar, e abundante em benignidade para todos os que te invocam.
6 Ee Bwana, sikia maombi yangu, sikiliza kilio changu unihurumie.
Dá ouvidos, Senhor, à minha oração, e atende à voz das minhas suplicas.
7 Katika siku ya shida yangu nitakuita, kwa maana wewe utanijibu.
No dia da minha angústia clamo a ti, porquanto me respondes.
8 Ee Bwana, katikati ya miungu hakuna kama wewe, hakuna matendo ya kulinganishwa na yako.
Entre os deuses não há semelhante a ti, Senhor, nem há obras como as tuas.
9 Ee Bwana, mataifa yote uliyoyafanya yatakuja na kuabudu mbele zako; wataliletea utukufu jina lako.
Todas as nações que fizeste virão e se prostrarão perante a tua face, Senhor, e glorificarão o teu nome
10 Kwa maana wewe ni mkuu, na unafanya mambo ya ajabu; wewe peke yako ndiwe Mungu.
Porque tu és grande e fazes maravilhas; só tu és Deus.
11 Ee Bwana, nifundishe njia yako, nami nitakwenda katika kweli yako; nipe moyo usiositasita, ili niweze kulicha jina lako.
Ensina-me, Senhor, o teu caminho, e andarei na tua verdade: une o meu coração ao temor do teu nome.
12 Ee Bwana wangu, nitakusifu kwa moyo wote; nitaliadhimisha jina lako milele.
Louvar-te-ei, Senhor Deus meu, com todo o meu coração, e glorificarei o teu nome para sempre.
13 Kwa maana upendo wako ni mkuu kwangu; umeniokoa kutoka kwenye vilindi vya kaburi. (Sheol h7585)
Pois grande é a tua misericórdia para comigo; e livraste a minha alma da sepultura mais profunda. (Sheol h7585)
14 Ee Mungu, wenye majivuno wananishambulia; kundi la watu wakatili linatafuta uhai wangu: watu wasiokuheshimu wewe.
Ó Deus, os soberbos se levantaram contra mim, e as assembléias dos tiranos procuraram a minha alma; e não te puseram perante os seus olhos.
15 Lakini wewe, Ee Bwana, ni Mungu wa huruma na neema, si mwepesi wa hasira, bali ni mwingi wa upendo na uaminifu.
Porém tu, Senhor, és um Deus cheio de compaixão, e piedoso, sofredor, e grande em benignidade e em verdade.
16 Nigeukie na unihurumie; mpe mtumishi wako nguvu zako, mwokoe mwana wa mtumishi wako wa kike.
Volta-te para mim, e tem misericórdia de mim; dá a tua fortaleza ao teu servo, e salva ao filho da tua serva.
17 Nipe ishara ya wema wako, ili adui zangu waione nao waaibishwe, kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umenisaidia na kunifariji.
Mostra-me um sinal para bem, para que o vejam aqueles que me aborrecem, e se confundam; porque tu, Senhor, me ajudaste e me consolaste.

< Zaburi 86 >