< Zaburi 86 >

1 Maombi ya Daudi. Ee Bwana, sikia na unijibu, kwa maana mimi ni maskini na mhitaji.
תפלה לדוד הטה יהוה אזנך ענני כי עני ואביון אני׃
2 Linda maisha yangu, kwa maana nimejiweka kwako, wewe ni Mungu wangu, mwokoe mtumishi wako anayekutumaini.
שמרה נפשי כי חסיד אני הושע עבדך אתה אלהי הבוטח אליך׃
3 Ee Bwana, nihurumie mimi, kwa maana ninakuita mchana kutwa.
חנני אדני כי אליך אקרא כל היום׃
4 Mpe mtumishi wako furaha, kwa kuwa kwako wewe, Ee Bwana, ninainua nafsi yangu.
שמח נפש עבדך כי אליך אדני נפשי אשא׃
5 Ee Bwana, wewe ni mwema na mwenye kusamehe, umejaa upendo kwa wote wakuitao.
כי אתה אדני טוב וסלח ורב חסד לכל קראיך׃
6 Ee Bwana, sikia maombi yangu, sikiliza kilio changu unihurumie.
האזינה יהוה תפלתי והקשיבה בקול תחנונותי׃
7 Katika siku ya shida yangu nitakuita, kwa maana wewe utanijibu.
ביום צרתי אקראך כי תענני׃
8 Ee Bwana, katikati ya miungu hakuna kama wewe, hakuna matendo ya kulinganishwa na yako.
אין כמוך באלהים אדני ואין כמעשיך׃
9 Ee Bwana, mataifa yote uliyoyafanya yatakuja na kuabudu mbele zako; wataliletea utukufu jina lako.
כל גוים אשר עשית יבואו וישתחוו לפניך אדני ויכבדו לשמך׃
10 Kwa maana wewe ni mkuu, na unafanya mambo ya ajabu; wewe peke yako ndiwe Mungu.
כי גדול אתה ועשה נפלאות אתה אלהים לבדך׃
11 Ee Bwana, nifundishe njia yako, nami nitakwenda katika kweli yako; nipe moyo usiositasita, ili niweze kulicha jina lako.
הורני יהוה דרכך אהלך באמתך יחד לבבי ליראה שמך׃
12 Ee Bwana wangu, nitakusifu kwa moyo wote; nitaliadhimisha jina lako milele.
אודך אדני אלהי בכל לבבי ואכבדה שמך לעולם׃
13 Kwa maana upendo wako ni mkuu kwangu; umeniokoa kutoka kwenye vilindi vya kaburi. (Sheol h7585)
כי חסדך גדול עלי והצלת נפשי משאול תחתיה׃ (Sheol h7585)
14 Ee Mungu, wenye majivuno wananishambulia; kundi la watu wakatili linatafuta uhai wangu: watu wasiokuheshimu wewe.
אלהים זדים קמו עלי ועדת עריצים בקשו נפשי ולא שמוך לנגדם׃
15 Lakini wewe, Ee Bwana, ni Mungu wa huruma na neema, si mwepesi wa hasira, bali ni mwingi wa upendo na uaminifu.
ואתה אדני אל רחום וחנון ארך אפים ורב חסד ואמת׃
16 Nigeukie na unihurumie; mpe mtumishi wako nguvu zako, mwokoe mwana wa mtumishi wako wa kike.
פנה אלי וחנני תנה עזך לעבדך והושיעה לבן אמתך׃
17 Nipe ishara ya wema wako, ili adui zangu waione nao waaibishwe, kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umenisaidia na kunifariji.
עשה עמי אות לטובה ויראו שנאי ויבשו כי אתה יהוה עזרתני ונחמתני׃

< Zaburi 86 >