< Zaburi 85 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Ee Bwana, ulionyesha wema kwa nchi yako. Ulimrejeshea Yakobo baraka zake.
Untuk pemimpin kor. Mazmur kaum Korah. Engkau berkenan kepada tanah-Mu, ya TUHAN, keadaan Israel sudah Kaupulihkan.
2 Ulisamehe uovu wa watu wako, na kufunika dhambi zao zote.
Engkau sudah mengampuni dosa-dosa umat-Mu; Kaumaafkan segala kesalahannya.
3 Uliweka kando ghadhabu yako yote na umegeuka na kuiacha hasira yako kali.
Mereka tidak lagi Kaumarahi; murka-Mu yang dahsyat Kautarik kembali.
4 Ee Mungu Mwokozi wetu, uturejeshe tena, nawe uiondoe chuki yako juu yetu.
Pulihkanlah kami, ya Allah penyelamat kami, jangan murka lagi kepada kami.
5 Je, utatukasirikia milele? Utaendeleza hasira yako kwa vizazi vyote?
Untuk selamanyakah Engkau memarahi kami, dan tetap marah turun-temurun?
6 Je, hutatuhuisha tena, ili watu wako wakufurahie?
Kuatkanlah kami kembali supaya kami umat-Mu bergembira karena pertolongan-Mu.
7 Utuonyeshe upendo wako usiokoma, Ee Bwana, utupe wokovu wako.
Tunjukkanlah bahwa Engkau tetap mengasihi, ya TUHAN, berilah kami keselamatan daripada-Mu.
8 Nitasikiliza lile atakalosema Mungu aliye Bwana; anaahidi amani kwa watu wake, watakatifu wake: lakini nao wasirudie upumbavu.
Aku mau mendengar perkataan TUHAN Allah; Ia menjanjikan kesejahteraan kepada kita, umat-Nya, asal kita tidak kembali berbuat dosa.
9 Hakika wokovu wake uko karibu na wale wamchao, ili utukufu wake udumu katika nchi yetu.
Sungguh, Ia siap menyelamatkan orang yang takwa, Allah yang agung akan berdiam di negeri kita.
10 Upendo na uaminifu hukutana pamoja, haki na amani hubusiana.
Kasih dan kesetiaan akan bertemu, keadilan dan damai akan berpeluk-pelukan.
11 Uaminifu huchipua kutoka nchi, haki hutazama chini kutoka mbinguni.
Kesetiaan manusia akan tumbuh dari bumi, dan keadilan Allah menjenguk dari langit.
12 Naam, hakika Bwana atatoa kilicho chema, nayo nchi yetu itazaa mavuno yake.
TUHAN mengaruniakan yang baik, maka tanah kita akan memberikan hasilnya.
13 Haki itatangulia mbele yake na kutengeneza njia kwa ajili ya hatua zake.
Keadilan akan mendahului TUHAN, dan menyiapkan jalan bagi-Nya.

< Zaburi 85 >