< Zaburi 84 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya wana wa Kora. Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, makao yako yapendeza kama nini!
Au maître chantre. En githith. Cantique des fils de Coré. Que tes demeures sont aimables, Éternel des armées!
2 Nafsi yangu inatamani sana, naam, hata kuona shauku, kwa ajili ya nyua za Bwana; moyo wangu na mwili wangu vinamlilia Mungu Aliye Hai.
Mon cœur se pâme, il languit après les parvis de l'Éternel; mon âme et ma chair crient au Dieu vivant.
3 Hata shomoro amejipatia makao, mbayuwayu amejipatia kiota mahali awezapo kuweka makinda yake: mahali karibu na madhabahu yako, Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mfalme wangu na Mungu wangu.
Le passereau même se trouve une demeure, et l'hirondelle un nid, où ils déposent leur couvée, près de tes autels, Éternel des armées, mon Roi et mon Dieu!
4 Heri wale wanaokaa nyumbani mwako, wanaokusifu wewe daima.
Heureux les habitants de ta maison! Ils te louent encore. (Pause)
5 Heri wale ambao nguvu zao ziko kwako, na njia ziendazo Sayuni zimo mioyoni mwao.
Heureux l'homme dont tu es le soutien, et que son cœur porte à s'acheminer vers toi!
6 Wanapopita katika Bonde la Baka, hulifanya mahali pa chemchemi, pia mvua za vuli hulijaza kwa madimbwi.
Traversant la vallée des pleurs, il la trouve pour lui arrosée de fontaines, et la pluie d'automne la couvre d'abondance.
7 Huendelea toka nguvu hadi nguvu, hadi kila mmoja afikapo mbele za Mungu huko Sayuni.
Il chemine, et ses forces augmentent: il se présente enfin devant Dieu en Sion.
8 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, sikia maombi yangu; nisikilize, Ee Mungu wa Yakobo.
Éternel, Dieu des armées, écoute ma prière! Prête l'oreille, Dieu de Jacob! (Pause)
9 Ee Mungu, uitazame ngao yetu, mtazame kwa wema mpakwa mafuta wako.
O notre bouclier, regarde, ô Dieu, abaisse un regard sur la face de ton Oint!
10 Siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu mahali pengine; afadhali ningekuwa bawabu katika nyumba ya Mungu wangu kuliko kukaa katika mahema ya waovu.
Car mieux vaut un jour dans tes parvis, que mille autres; j'aime mieux me tenir au seuil de la maison de mon Dieu, que d'habiter les tentes de l'impiété.
11 Kwa kuwa Bwana ni jua na ngao, Bwana hutoa wema na heshima; hakuna kitu chema anachowanyima wale ambao hawana hatia.
Car l'Éternel Dieu est un soleil et un bouclier, l'Éternel donne grâce et magnificence, ne refuse aucun bien à qui suit la droiture.
12 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, heri ni mtu yule anayekutumaini wewe.
Éternel des armées, heureux l'homme qui se confie en toi!

< Zaburi 84 >