< Zaburi 84 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya wana wa Kora. Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, makao yako yapendeza kama nini!
Éternel des armées, que tes tabernacles sont aimables!
2 Nafsi yangu inatamani sana, naam, hata kuona shauku, kwa ajili ya nyua za Bwana; moyo wangu na mwili wangu vinamlilia Mungu Aliye Hai.
Mon âme languit, même elle se consume après les parvis de l'Éternel; mon cœur et ma chair crient vers le Dieu vivant.
3 Hata shomoro amejipatia makao, mbayuwayu amejipatia kiota mahali awezapo kuweka makinda yake: mahali karibu na madhabahu yako, Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mfalme wangu na Mungu wangu.
Le passereau même a bien trouvé une maison, et l'hirondelle son nid où elle a mis ses petits. Tes autels, ô Éternel des armées, mon roi et mon Dieu!
4 Heri wale wanaokaa nyumbani mwako, wanaokusifu wewe daima.
Heureux ceux qui habitent ta maison, qui te louent incessamment! (Sélah, pause)
5 Heri wale ambao nguvu zao ziko kwako, na njia ziendazo Sayuni zimo mioyoni mwao.
Heureux l'homme dont la force est en toi, ceux qui aiment les chemins de ta maison!
6 Wanapopita katika Bonde la Baka, hulifanya mahali pa chemchemi, pia mvua za vuli hulijaza kwa madimbwi.
Passant par la vallée de Baca (Larmes), ils en font une source vive; et la pluie d'automne la couvre de biens.
7 Huendelea toka nguvu hadi nguvu, hadi kila mmoja afikapo mbele za Mungu huko Sayuni.
Ils vont de force en force pour se présenter devant Dieu en Sion.
8 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, sikia maombi yangu; nisikilize, Ee Mungu wa Yakobo.
Éternel, Dieu des armées, écoute ma prière! Dieu de Jacob, prête l'oreille!
9 Ee Mungu, uitazame ngao yetu, mtazame kwa wema mpakwa mafuta wako.
O Dieu, notre bouclier, vois et regarde la face de ton Oint!
10 Siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu mahali pengine; afadhali ningekuwa bawabu katika nyumba ya Mungu wangu kuliko kukaa katika mahema ya waovu.
Car un jour dans tes parvis vaut mieux que mille ailleurs. J'aime mieux me tenir sur le seuil, dans la maison de mon Dieu, que d'habiter dans les tentes des méchants.
11 Kwa kuwa Bwana ni jua na ngao, Bwana hutoa wema na heshima; hakuna kitu chema anachowanyima wale ambao hawana hatia.
Car l'Éternel Dieu est un soleil et un bouclier; l'Éternel donne la grâce et la gloire; il ne refuse aucun bien à ceux qui marchent dans l'intégrité.
12 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, heri ni mtu yule anayekutumaini wewe.
Éternel des armées, heureux l'homme qui se confie en toi!

< Zaburi 84 >