< Zaburi 84 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya wana wa Kora. Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, makao yako yapendeza kama nini!
Pour le chef musicien. Sur un instrument de Gath. Un psaume par les fils de Korah. Que tes demeures sont belles! Yahvé des Armées!
2 Nafsi yangu inatamani sana, naam, hata kuona shauku, kwa ajili ya nyua za Bwana; moyo wangu na mwili wangu vinamlilia Mungu Aliye Hai.
Mon âme soupire, et même s'évanouit, pour les parvis de l'Éternel. Mon cœur et ma chair crient pour le Dieu vivant.
3 Hata shomoro amejipatia makao, mbayuwayu amejipatia kiota mahali awezapo kuweka makinda yake: mahali karibu na madhabahu yako, Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mfalme wangu na Mungu wangu.
Oui, le moineau a trouvé une maison, et l'hirondelle un nid pour elle, où elle pourra avoir ses petits, près de vos autels, Yahvé des armées, mon roi et mon Dieu.
4 Heri wale wanaokaa nyumbani mwako, wanaokusifu wewe daima.
Heureux ceux qui habitent dans ta maison. Ils te louent toujours. (Selah)
5 Heri wale ambao nguvu zao ziko kwako, na njia ziendazo Sayuni zimo mioyoni mwao.
Heureux ceux qui ont leur force en toi, qui ont choisi de faire un pèlerinage.
6 Wanapopita katika Bonde la Baka, hulifanya mahali pa chemchemi, pia mvua za vuli hulijaza kwa madimbwi.
En passant par la vallée des pleurs, ils en font un lieu de sources. Oui, la pluie d'automne la couvre de bénédictions.
7 Huendelea toka nguvu hadi nguvu, hadi kila mmoja afikapo mbele za Mungu huko Sayuni.
Ils vont de force en force. Chacun d'entre eux comparaît devant Dieu à Sion.
8 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, sikia maombi yangu; nisikilize, Ee Mungu wa Yakobo.
Yahvé, Dieu des armées, écoute ma prière. Écoute, Dieu de Jacob. (Selah)
9 Ee Mungu, uitazame ngao yetu, mtazame kwa wema mpakwa mafuta wako.
Voici Dieu, notre bouclier, regarde le visage de ton oint.
10 Siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu mahali pengine; afadhali ningekuwa bawabu katika nyumba ya Mungu wangu kuliko kukaa katika mahema ya waovu.
Car un jour dans tes tribunaux vaut mieux que mille. Je préfère être un portier dans la maison de mon Dieu, que d'habiter dans les tentes de la méchanceté.
11 Kwa kuwa Bwana ni jua na ngao, Bwana hutoa wema na heshima; hakuna kitu chema anachowanyima wale ambao hawana hatia.
Car Yahvé Dieu est un soleil et un bouclier. Yahvé donnera la grâce et la gloire. Il ne refuse aucun bien à ceux qui marchent sans reproche.
12 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, heri ni mtu yule anayekutumaini wewe.
Yahvé des Armées, Heureux l'homme qui a confiance en toi.

< Zaburi 84 >