< Zaburi 84 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya wana wa Kora. Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, makao yako yapendeza kama nini!
Veisuunjohtajalle; veisataan kuin viininkorjuulaulu; koorahilaisten virsi. Kuinka ihanat ovat sinun asuinsijasi, Herra Sebaot!
2 Nafsi yangu inatamani sana, naam, hata kuona shauku, kwa ajili ya nyua za Bwana; moyo wangu na mwili wangu vinamlilia Mungu Aliye Hai.
Minun sieluni ikävöitsee ja halajaa Herran esikartanoihin, minun sydämeni ja ruumiini pyrkii riemuiten elävää Jumalaa kohti.
3 Hata shomoro amejipatia makao, mbayuwayu amejipatia kiota mahali awezapo kuweka makinda yake: mahali karibu na madhabahu yako, Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mfalme wangu na Mungu wangu.
Löysihän lintunen majan ja pääskynen pesän, johon se poikasensa laskee: sinun alttarisi, Herra Sebaot, minun kuninkaani ja minun Jumalani.
4 Heri wale wanaokaa nyumbani mwako, wanaokusifu wewe daima.
Autuaat ne, jotka sinun huoneessasi asuvat! He kiittävät sinua alati. (Sela)
5 Heri wale ambao nguvu zao ziko kwako, na njia ziendazo Sayuni zimo mioyoni mwao.
Autuaat ne ihmiset, joilla on voimansa sinussa, joilla on mielessänsä pyhät matkat!
6 Wanapopita katika Bonde la Baka, hulifanya mahali pa chemchemi, pia mvua za vuli hulijaza kwa madimbwi.
Kun he käyvät Kyynellaakson kautta, he muuttavat sen lähteitten maaksi, ja syyssade peittää sen siunauksilla.
7 Huendelea toka nguvu hadi nguvu, hadi kila mmoja afikapo mbele za Mungu huko Sayuni.
He käyvät voimasta voimaan, he astuvat Jumalan eteen Siionissa.
8 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, sikia maombi yangu; nisikilize, Ee Mungu wa Yakobo.
Herra, Jumala Sebaot, kuule minun rukoukseni, ota se korviisi, Jaakobin Jumala. (Sela)
9 Ee Mungu, uitazame ngao yetu, mtazame kwa wema mpakwa mafuta wako.
Jumala, meidän kilpemme, käännä katseesi, katso voideltusi kasvoja.
10 Siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu mahali pengine; afadhali ningekuwa bawabu katika nyumba ya Mungu wangu kuliko kukaa katika mahema ya waovu.
Sillä yksi päivä sinun esikartanoissasi on parempi kuin tuhat muualla; mieluummin minä olen vartijana Jumalani huoneen kynnyksellä, kuin asun jumalattomien majoissa.
11 Kwa kuwa Bwana ni jua na ngao, Bwana hutoa wema na heshima; hakuna kitu chema anachowanyima wale ambao hawana hatia.
Sillä Herra Jumala on aurinko ja kilpi; Herra antaa armon ja kunnian, ei hän kiellä hyvää niiltä, jotka nuhteettomasti vaeltavat.
12 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, heri ni mtu yule anayekutumaini wewe.
Herra Sebaot, autuas se ihminen, joka sinuun turvaa!