< Zaburi 84 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya wana wa Kora. Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, makao yako yapendeza kama nini!
TO THE OVERSEER. ON THE GITTITH. A PSALM OF THE SONS OF KORAH. How beloved Your dwelling places, YHWH of Hosts!
2 Nafsi yangu inatamani sana, naam, hata kuona shauku, kwa ajili ya nyua za Bwana; moyo wangu na mwili wangu vinamlilia Mungu Aliye Hai.
My soul desired, indeed, it has also been consumed, For the courts of YHWH, My heart and my flesh cry aloud to the living God,
3 Hata shomoro amejipatia makao, mbayuwayu amejipatia kiota mahali awezapo kuweka makinda yake: mahali karibu na madhabahu yako, Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mfalme wangu na Mungu wangu.
Even a sparrow has found a house, And a swallow a nest for herself, Where she has placed her brood—Your altars, O YHWH of Hosts, My king and my God.
4 Heri wale wanaokaa nyumbani mwako, wanaokusifu wewe daima.
O the blessedness of those inhabiting Your house, Yet they praise You. (Selah)
5 Heri wale ambao nguvu zao ziko kwako, na njia ziendazo Sayuni zimo mioyoni mwao.
O the blessedness of a man whose strength is in You, Highways [are] in their heart.
6 Wanapopita katika Bonde la Baka, hulifanya mahali pa chemchemi, pia mvua za vuli hulijaza kwa madimbwi.
Those passing through a valley of weeping make it a spring, The early rain covers it with pools.
7 Huendelea toka nguvu hadi nguvu, hadi kila mmoja afikapo mbele za Mungu huko Sayuni.
They go from strength to strength, He appears to God in Zion.
8 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, sikia maombi yangu; nisikilize, Ee Mungu wa Yakobo.
O YHWH, God of Hosts, hear my prayer, Give ear, O God of Jacob. (Selah)
9 Ee Mungu, uitazame ngao yetu, mtazame kwa wema mpakwa mafuta wako.
Our shield, see, O God, And behold the face of Your anointed,
10 Siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu mahali pengine; afadhali ningekuwa bawabu katika nyumba ya Mungu wangu kuliko kukaa katika mahema ya waovu.
For a day in Your courts [is] good, O Teacher! I have chosen rather to be at the threshold, In the house of my God, Than to dwell in tents of wickedness.
11 Kwa kuwa Bwana ni jua na ngao, Bwana hutoa wema na heshima; hakuna kitu chema anachowanyima wale ambao hawana hatia.
For YHWH God [is] a sun and a shield, YHWH gives grace and glory. He does not withhold good To those walking in uprightness.
12 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, heri ni mtu yule anayekutumaini wewe.
YHWH of Hosts! O the blessedness of a man trusting in You.