< Zaburi 84 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya wana wa Kora. Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, makao yako yapendeza kama nini!
Unto the end, for the winepresses, a psalm for the sons of Core. How lovely are thy tabernacles, O Lord of host!
2 Nafsi yangu inatamani sana, naam, hata kuona shauku, kwa ajili ya nyua za Bwana; moyo wangu na mwili wangu vinamlilia Mungu Aliye Hai.
My soul longeth and fainteth for the courts of the Lord. My heart and my flesh have rejoiced in the living God.
3 Hata shomoro amejipatia makao, mbayuwayu amejipatia kiota mahali awezapo kuweka makinda yake: mahali karibu na madhabahu yako, Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mfalme wangu na Mungu wangu.
For the sparrow hath found herself a house, and the turtle a nest for herself where she may lay her young ones: Thy altars, O Lord of hosts, my king and my God.
4 Heri wale wanaokaa nyumbani mwako, wanaokusifu wewe daima.
Blessed are they that dwell in thy house, O Lord: they shall praise thee for ever and ever.
5 Heri wale ambao nguvu zao ziko kwako, na njia ziendazo Sayuni zimo mioyoni mwao.
Blessed is the man whose help is from thee: in his heart he hath disposed to ascend by steps,
6 Wanapopita katika Bonde la Baka, hulifanya mahali pa chemchemi, pia mvua za vuli hulijaza kwa madimbwi.
In the vale of tears, in the place which be hath set.
7 Huendelea toka nguvu hadi nguvu, hadi kila mmoja afikapo mbele za Mungu huko Sayuni.
For the lawgiver shall give a blessing, they shall go from virtue to virtue: the God of gods shall be seen in Sion.
8 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, sikia maombi yangu; nisikilize, Ee Mungu wa Yakobo.
O Lord God of hosts, hear my prayer: give ear, O God of Jacob.
9 Ee Mungu, uitazame ngao yetu, mtazame kwa wema mpakwa mafuta wako.
Behold, O God our protector: and look on the face of thy Christ.
10 Siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu mahali pengine; afadhali ningekuwa bawabu katika nyumba ya Mungu wangu kuliko kukaa katika mahema ya waovu.
For better is one day in thy courts above thousands. I have chosen to be an abject in the house of my God, rather than to dwell in the tabernacles of sinners.
11 Kwa kuwa Bwana ni jua na ngao, Bwana hutoa wema na heshima; hakuna kitu chema anachowanyima wale ambao hawana hatia.
For God loveth mercy and truth: the Lord will give grace and glory.
12 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, heri ni mtu yule anayekutumaini wewe.
He will not deprive of good things them that walk in innocence: O Lord of hosts, blessed is the man that trusteth in thee.

< Zaburi 84 >