< Zaburi 84 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya wana wa Kora. Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, makao yako yapendeza kama nini!
How amiable are thy tabernacles, O Jehovah of hosts!
2 Nafsi yangu inatamani sana, naam, hata kuona shauku, kwa ajili ya nyua za Bwana; moyo wangu na mwili wangu vinamlilia Mungu Aliye Hai.
My soul longs, yea, even faints for the courts of Jehovah. My heart and my flesh cry out to the living God.
3 Hata shomoro amejipatia makao, mbayuwayu amejipatia kiota mahali awezapo kuweka makinda yake: mahali karibu na madhabahu yako, Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mfalme wangu na Mungu wangu.
Yea, the sparrow has found her a house, and the swallow a nest for herself where she may lay her young, even thine altars, O Jehovah of hosts, my King and my God.
4 Heri wale wanaokaa nyumbani mwako, wanaokusifu wewe daima.
Blessed are those who dwell in thy house. They will still be praising thee. (Selah)
5 Heri wale ambao nguvu zao ziko kwako, na njia ziendazo Sayuni zimo mioyoni mwao.
Blessed is the man whose strength is in thee, in whose heart are the highways to Zion.
6 Wanapopita katika Bonde la Baka, hulifanya mahali pa chemchemi, pia mvua za vuli hulijaza kwa madimbwi.
Passing through the valley of weeping they make it a place of springs. Yea, the early rain covers it with blessings.
7 Huendelea toka nguvu hadi nguvu, hadi kila mmoja afikapo mbele za Mungu huko Sayuni.
They go from strength to strength; each one of them appears before God in Zion.
8 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, sikia maombi yangu; nisikilize, Ee Mungu wa Yakobo.
O Jehovah God of hosts, hear my prayer. Give ear, O God of Jacob. (Selah)
9 Ee Mungu, uitazame ngao yetu, mtazame kwa wema mpakwa mafuta wako.
Behold, O God our shield, and look upon the face of thine anointed.
10 Siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu mahali pengine; afadhali ningekuwa bawabu katika nyumba ya Mungu wangu kuliko kukaa katika mahema ya waovu.
For a day in thy courts is better than a thousand. I had rather be a doorkeeper in the house of my God, than to dwell in the tents of wickedness.
11 Kwa kuwa Bwana ni jua na ngao, Bwana hutoa wema na heshima; hakuna kitu chema anachowanyima wale ambao hawana hatia.
For Jehovah God is a sun and a shield. Jehovah will give grace and glory. He will withhold no good thing from those who walk uprightly.
12 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, heri ni mtu yule anayekutumaini wewe.
O Jehovah of hosts, blessed is the man who trusts in thee.