< Zaburi 84 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya wana wa Kora. Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, makao yako yapendeza kama nini!
Zborovođi. Po napjevu “Tijesci”. Sinova Korahovih. Kako su mili stanovi tvoji, Jahve nad Vojskama!
2 Nafsi yangu inatamani sana, naam, hata kuona shauku, kwa ajili ya nyua za Bwana; moyo wangu na mwili wangu vinamlilia Mungu Aliye Hai.
Duša mi gine i čezne za dvorima Jahvinim. Srce moje i moje tijelo kliču Bogu živomu.
3 Hata shomoro amejipatia makao, mbayuwayu amejipatia kiota mahali awezapo kuweka makinda yake: mahali karibu na madhabahu yako, Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mfalme wangu na Mungu wangu.
I vrabac sebi log nalazi, i lastavica gnjezdašce gdje će položiti mlade svoje:
4 Heri wale wanaokaa nyumbani mwako, wanaokusifu wewe daima.
a ja žrtvenike tvoje, Jahve nad Vojskama, Kralju moj i Bože moj! Blaženi koji prebivaju u Domu tvome slaveć' te bez prestanka!
5 Heri wale ambao nguvu zao ziko kwako, na njia ziendazo Sayuni zimo mioyoni mwao.
Blažen komu je pomoć u tebi dok se sprema na svete putove!
6 Wanapopita katika Bonde la Baka, hulifanya mahali pa chemchemi, pia mvua za vuli hulijaza kwa madimbwi.
Prolaze li suhom dolinom, u izvor je vode promeću i prva je kiša u blagoslov odijeva.
7 Huendelea toka nguvu hadi nguvu, hadi kila mmoja afikapo mbele za Mungu huko Sayuni.
Snaga im raste od časa do časa: dok ne ugledaju Boga na Sionu.
8 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, sikia maombi yangu; nisikilize, Ee Mungu wa Yakobo.
Jahve, Bože nad Vojskama, čuj molitvu moju, poslušaj, Bože Jakovljev!
9 Ee Mungu, uitazame ngao yetu, mtazame kwa wema mpakwa mafuta wako.
Pogledaj, štite naš, Bože, pogledaj lice pomazanika svoga!
10 Siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu mahali pengine; afadhali ningekuwa bawabu katika nyumba ya Mungu wangu kuliko kukaa katika mahema ya waovu.
Zaista, jedan je dan u dvorima tvojim bolji od tisuću drugih. Volim biti na pragu Doma Boga svoga nego boraviti u šatorima grešnika.
11 Kwa kuwa Bwana ni jua na ngao, Bwana hutoa wema na heshima; hakuna kitu chema anachowanyima wale ambao hawana hatia.
Jahve, Bog, sunce je i štit: on daje milost i slavu. Ne uskraćuje Jahve dobara onima koji idu u nedužnosti.
12 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, heri ni mtu yule anayekutumaini wewe.
Jahve nad Vojskama, blago onom tko se u te uzda.

< Zaburi 84 >