< Zaburi 84 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya wana wa Kora. Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, makao yako yapendeza kama nini!
Kathutkung: Korah capanaw Oe ransahu BAWIPA, na onae teh banghloimaw ngai ao.
2 Nafsi yangu inatamani sana, naam, hata kuona shauku, kwa ajili ya nyua za Bwana; moyo wangu na mwili wangu vinamlilia Mungu Aliye Hai.
Ka hringnae ni a rabui, Bokheiyah, BAWIPA thongma rabui laihoi ka tâwn. Ka lungthin hoi ka takthai ni kahring Cathut teh atangcalah a kaw.
3 Hata shomoro amejipatia makao, mbayuwayu amejipatia kiota mahali awezapo kuweka makinda yake: mahali karibu na madhabahu yako, Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mfalme wangu na Mungu wangu.
Oe ransahu BAWIPA, ka Siangpahrang hoi ka Cathut, na thuengnae khoungroe dawk pusu ni tabu a tuk teh, pingpit ni hai a canaw ta nahanelah tabu a tuk.
4 Heri wale wanaokaa nyumbani mwako, wanaokusifu wewe daima.
Na im dawk kaawmnaw teh, a yaw kahawi e doeh. Pou na pholen awh han. (Selah)
5 Heri wale ambao nguvu zao ziko kwako, na njia ziendazo Sayuni zimo mioyoni mwao.
Nang thaonae lah ka hnonaw hoi hmuen ka thoung koe cei ngainae lungthin ka tawn naw teh tami a yaw kahawi e doeh.
6 Wanapopita katika Bonde la Baka, hulifanya mahali pa chemchemi, pia mvua za vuli hulijaza kwa madimbwi.
Baca yawn dawk a cei awh navah, tuiphuek tâconae lah a coung sak teh, khotui hai a kamuem sak.
7 Huendelea toka nguvu hadi nguvu, hadi kila mmoja afikapo mbele za Mungu huko Sayuni.
Thaonae koehoi thathoenae koe lah cei awh teh, buet touh hnukkhu buet touh Zion Cathut hmalah a kamnue awh.
8 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, sikia maombi yangu; nisikilize, Ee Mungu wa Yakobo.
Oe ransahu Cathut BAWIPA, ka ratoumnae heh na thai pouh haw. Oe, Jakop Cathut, na hnâpakeng haw.
9 Ee Mungu, uitazame ngao yetu, mtazame kwa wema mpakwa mafuta wako.
Oe Cathut, ka bahling khen nateh, Satui na awi e mei hah khenhaw!
10 Siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu mahali pengine; afadhali ningekuwa bawabu katika nyumba ya Mungu wangu kuliko kukaa katika mahema ya waovu.
Bangkongtetpawiteh, na thongma dawk hnin touh o e teh, alouklah hnin 1,000 touh o e hlak ahawihnawn. Thoenae rim dawk o e hlak teh Cathut im longkha ring e ka ngaihnawn.
11 Kwa kuwa Bwana ni jua na ngao, Bwana hutoa wema na heshima; hakuna kitu chema anachowanyima wale ambao hawana hatia.
Bangkongtetpawiteh, BAWIPA Cathut teh kanî hoi bahling doeh. BAWIPA ni lungmanae hoi bawilennae a poe han.
12 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, heri ni mtu yule anayekutumaini wewe.
Oe ransahu BAWIPA, nang kâuep e teh a yaw kahawi e doeh.

< Zaburi 84 >