< Zaburi 82 >

1 Zaburi ya Asafu. Mungu anaongoza kusanyiko kuu, anatoa hukumu miongoni mwa “miungu”:
מזמור לאסף אלהים נצב בעדת-אל בקרב אלהים ישפט
2 “Hata lini utaendelea kuwatetea wasio haki na kuonyesha upendeleo kwa waovu?
עד-מתי תשפטו-עול ופני רשעים תשאו-סלה
3 Teteeni wanyonge na yatima, tunzeni haki za maskini na walioonewa.
שפטו-דל ויתום עני ורש הצדיקו
4 Mwokoeni mnyonge na mhitaji, wakomboeni kutoka mkononi mwa mwovu.
פלטו-דל ואביון מיד רשעים הצילו
5 “Hawajui lolote, hawaelewi lolote. Wanatembea gizani; misingi yote ya dunia imetikisika.
לא ידעו ולא יבינו-- בחשכה יתהלכו ימוטו כל-מוסדי ארץ
6 “Nilisema, ‘Ninyi ni “miungu”; ninyi nyote ni wana wa Aliye Juu Sana.’
אני-אמרתי אלהים אתם ובני עליון כלכם
7 Lakini mtakufa kama wanadamu wa kawaida; mtaanguka kama mtawala mwingine yeyote.”
אכן כאדם תמותון וכאחד השרים תפלו
8 Ee Mungu, inuka uihukumu nchi, kwa kuwa mataifa yote ni urithi wako.
קומה אלהים שפטה הארץ כי-אתה תנחל בכל-הגוים

< Zaburi 82 >