< Zaburi 81 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
Начальнику хора. На Гефском орудии. Псалом Асафа. Радостно пойте Богу, твердыне нашей; восклицайте Богу Иакова;
2 Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
возьмите псалом, дайте тимпан, сладкозвучные гусли с псалтирью;
3 Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
трубите в новомесячие трубою, в определенное время, в день праздника нашего;
4 hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
ибо это закон для Израиля, устав от Бога Иаковлева.
5 Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
Он установил это во свидетельство для Иосифа, когда он вышел из земли Египетской, где услышал звуки языка, которого не знал:
6 Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
“Я снял с рамен его тяжести, и руки его освободились от корзин.
7 Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
В бедствии ты призвал Меня, и Я избавил тебя; из среды грома Я услышал тебя, при водах Меривы испытал тебя.
8 “Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
Слушай, народ Мой, и Я буду свидетельствовать тебе: Израиль! о, если бы ты послушал Меня!
9 Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
Да не будет у тебя иного бога, и не поклоняйся богу чужеземному.
10 Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
Я Господь, Бог твой, изведший тебя из земли Египетской; открой уста твои, и Я наполню их”.
11 “Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
Но народ Мой не слушал гласа Моего, и Израиль не покорялся Мне;
12 Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
потому Я оставил их упорству сердца их, пусть ходят по своим помыслам.
13 “Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
О, если бы народ Мой слушал Меня и Израиль ходил Моими путями!
14 ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
Я скоро смирил бы врагов их и обратил бы руку Мою на притеснителей их:
15 Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
ненавидящие Господа раболепствовали бы им, а их благоденствие продолжалось бы навсегда;
16 Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”
Я питал бы их туком пшеницы и насыщал бы их медом из скалы.