< Zaburi 81 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
Til sangmesteren, efter Gittit; av Asaf. Juble for Gud, vår styrke, rop med glede for Jakobs Gud!
2 Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
Stem i sang og la pauken lyde, den liflige citar tillikemed harpen!
3 Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
Støt i basun i måneden, ved fullmånen, på vår høitids dag!
4 hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
For det er en lov for Israel, en rett for Jakobs Gud.
5 Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
Han satte det til et vidnesbyrd i Josef da han drog ut gjennem Egyptens land. - Jeg hørte en røst som jeg ikke kjente:
6 Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
Jeg fridde hans skulder fra byrden, hans hender slapp fri fra bærekurven.
7 Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
I nøden ropte du, og jeg fridde dig ut; jeg svarte dig, skjult i tordenskyen, jeg prøvde dig ved Meriba-vannene. (Sela)
8 “Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
Hør, mitt folk, og jeg vil vidne for dig! Israel, o, at du vilde høre mig:
9 Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
Det skal ikke være nogen fremmed gud hos dig, og du skal ikke tilbede utlendingens gud.
10 Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
Jeg er Herren din Gud, som førte dig op av Egyptens land; lukk din munn vidt op, at jeg kan fylle den!
11 “Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
Men mitt folk hørte ikke min røst, og Israel vilde ikke lyde mig.
12 Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
Så lot jeg dem fare i sitt hjertes hårdhet, forat de skulde vandre i sine egne onde råd.
13 “Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
O, at mitt folk vilde høre mig, og at Israel vilde vandre på mine veier!
14 ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
Om en liten stund vilde jeg da ydmyke deres fiender og vende min hånd imot deres motstandere.
15 Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
De som hater Herren, skulde smigre for dem, og deres tid skulde vare evindelig.
16 Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”
Og han skulde fø dem med den beste hvete, og jeg skulde mette dig med honning fra klippen.

< Zaburi 81 >