< Zaburi 81 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
Untuk pemimpin kor. Menurut lagu: Gitit. Dari Asaf. Nyanyikanlah puji-pujian bagi Allah, kekuatan kita, bersoraklah dengan gembira bagi Allah Yakub.
2 Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
Bunyikanlah rebana, angkatlah lagu, petiklah gambus dan kecapi dengan merdu.
3 Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
Tiuplah terompet pada hari raya kita, pada pesta bulan baru dan bulan purnama.
4 hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
Sebab hal itu suatu peraturan di Israel, suatu perintah dari Allah Yakub.
5 Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
Ia menjadikannya sebuah ketetapan bagi bangsa Israel, ketika Ia maju melawan Mesir. Aku mendengar bahasa yang tidak kukenal,
6 Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
"Aku telah mengangkat beban dari pundakmu, dan melepaskan keranjang pikulan dari tanganmu.
7 Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
Dalam kesusahanmu kamu berseru, dan Aku menyelamatkan kamu. Kujawab kamu dari guntur tempat Aku bersembunyi, Kuuji kamu di mata air Meriba.
8 “Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
Dengarlah peringatan-Ku, hai umat-Ku, Israel, sekiranya kamu mau mendengarkan Aku!
9 Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
Jangan di antaramu ada ilah lain, janganlah menyembah ilah asing.
10 Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
Akulah TUHAN Allahmu, yang menuntun kamu keluar dari Mesir. Waktu kamu lapar kamu Kuberi makan.
11 “Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
Tapi umat-Ku tak mau mendengarkan Aku, Israel tak mau taat kepada-Ku.
12 Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
Sebab itu Aku membiarkan mereka berkeras kepala; biarlah mereka mengikuti kemauan mereka sendiri.
13 “Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
Ah, sekiranya umat-Ku mau mendengarkan Aku, sekiranya mereka mau taat kepada-Ku,
14 ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
maka Aku segera menundukkan musuh mereka, dan mengalahkan semua lawan mereka.
15 Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
Orang yang membenci Aku akan Kutaklukkan, mereka akan dihukum untuk selama-lamanya.
16 Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”
Tetapi umat-Ku akan Kuberi makan gandum pilihan, dan Kukenyangkan dengan madu hutan."