< Zaburi 81 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
Pour les pressoirs, psaume d’Asaph lui-même. Exultez en Dieu qui est notre aide; poussez des cris de joie vers le Dieu de Jacob.
2 Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
Entonnez un psaume, et faites entendre un tambour, un psaltérion harmonieux avec une harpe.
3 Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
Sonnez de la trompette à la néoménie, au jour insigne de votre solennité;
4 hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
Parce que c’est un précepte dans Israël, une ordonnance en l’honneur du Dieu de Jacob.
5 Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
Il l’établit comme un monument pour Joseph, lorsqu’il sortit de la terre d’Égypte, et qu’il entendit une langue qu’il ne connaissait pas.
6 Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
Il détourna son dos des fardeaux, et ses mains qui servaient à porter les corbeilles.
7 Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
Dans la tribulation, tu m’as invoqué, et je t’ai délivré; je t’ai exaucé du fond de la tempête, je t’ai éprouvé auprès de l’eau de contradiction.
8 “Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
Écoute, mon peuple, car je te prendrai à témoin: Israël, si tu m’écoutes,
9 Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
Il n’y aura pas au milieu de toi de dieu nouveau, et tu n’adoreras pas de dieu étranger.
10 Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
Car c’est moi qui suis le Seigneur ton Dieu, qui t’ai tiré de la terre d’Égypte; élargis la bouche, je la remplirai.
11 “Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
Mais mon peuple n’a pas écouté ma voix, et Israël ne m’a pas prêté attention.
12 Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
Et je les ai abandonnés aux désirs de leur cœur; ils iront dans des voies de leur invention.
13 “Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
Si mon peuple m’avait écouté; si Israël avait marché dans mes voies,
14 ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
En un moment j’aurais humilié ses ennemis, et sur ceux qui les tourmentaient, j’aurais lancé ma main.
15 Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
Les ennemis du Seigneur lui ont menti, et leur temps durera des siècles.
16 Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”
Cependant il les a nourris de moelle de froment, et il les a rassasiés de miel sorti d’une pierre.

< Zaburi 81 >