< Zaburi 81 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
Au maître-chantre. — D'Asaph. — Sur la Guittith. Chantez avec allégresse en l'honneur de Dieu, notre force; Jetez des cris de joie à la gloire du Dieu de Jacob!
2 Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
Entonnez un cantique, faites résonner le tambourin, La douce harpe, avec la lyre.
3 Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
Sonnez de la trompette, à la nouvelle lune, A la pleine lune, le jour de notre fête;
4 hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
Car c'est une loi pour Israël, Un commandement du Dieu de Jacob.
5 Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
C'est la règle qu'il établit parmi les fils de Joseph, Quand il exerça ses jugements contre le pays d'Egypte. J'entendis alors un langage que je ne connaissais pas:
6 Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
«J'ai déchargé de son fardeau ton épaule; Tes mains ne sont plus asservies à de durs labeurs.
7 Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
Dans ta détresse, tu as crié et je t'ai délivré. Du sein de la tempête dont j'étais enveloppé, J'ai exaucé tes prières; Je t'ai éprouvé aux eaux de Mériba. (Pause)
8 “Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
Écoute, ô mon peuple, et je t'instruirai! O Israël, si tu m'écoutais!
9 Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
Qu'il n'y ait au milieu de toi aucun dieu étranger; Ne te prosterne pas devant un autre dieu!
10 Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
Je suis l'Éternel, ton Dieu: Je t'ai fait remonter du pays d'Egypte. Ouvre ta bouche, et je la remplirai.»
11 “Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
Mais mon peuple n'a pas écouté ma voix; Les enfants d'Israël n'ont pas voulu m'obéir.
12 Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
Alors je les ai abandonnés à la dureté de leur coeur, Et ils ont marché au gré de leurs désirs.
13 “Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
Oh! si mon peuple voulait m'écouter, Si les enfants d'Israël marchaient dans mes voies!
14 ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
J'aurais bientôt abattu leurs ennemis; Je ferais peser ma main sur leurs adversaires!
15 Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
Ceux qui haïssent l'Éternel viendraient flatter son peuple; Sa prospérité durerait éternellement.
16 Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”
Je vous nourrirais de la moelle du froment; Je vous rassasierais encore du miel du rocher.

< Zaburi 81 >