< Zaburi 81 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
Au chef des chantres. Sur la guitthith. D’Asaph. Chantez avec allégresse à Dieu, notre force! Poussez des cris de joie vers le Dieu de Jacob!
2 Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
Entonnez des cantiques, faites résonner le tambourin, La harpe mélodieuse et le luth!
3 Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
Sonnez de la trompette à la nouvelle lune, A la pleine lune, au jour de notre fête!
4 hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
Car c’est une loi pour Israël, Une ordonnance du Dieu de Jacob.
5 Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
Il en fit un statut pour Joseph, Quand il marcha contre le pays d’Égypte… J’entends une voix qui m’est inconnue:
6 Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
J’ai déchargé son épaule du fardeau, Et ses mains ont lâché la corbeille.
7 Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
Tu as crié dans la détresse, et je t’ai délivré; Je t’ai répondu dans la retraite du tonnerre; Je t’ai éprouvé près des eaux de Meriba. (Pause)
8 “Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
Écoute, mon peuple! Et je t’avertirai; Israël, puisses-tu m’écouter!
9 Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
Qu’il n’y ait au milieu de toi point de dieu étranger! Ne te prosterne pas devant des dieux étrangers!
10 Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
Je suis l’Éternel, ton Dieu, qui t’ai fait monter du pays d’Égypte; Ouvre ta bouche, et je la remplirai.
11 “Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
Mais mon peuple n’a point écouté ma voix, Israël ne m’a point obéi.
12 Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
Alors je les ai livrés aux penchants de leur cœur, Et ils ont suivi leurs propres conseils.
13 “Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
Oh! Si mon peuple m’écoutait, Si Israël marchait dans mes voies!
14 ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
En un instant je confondrais leurs ennemis, Je tournerais ma main contre leurs adversaires;
15 Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
Ceux qui haïssent l’Éternel le flatteraient, Et le bonheur d’Israël durerait toujours;
16 Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”
Je le nourrirais du meilleur froment, Et je le rassasierais du miel du rocher.