< Zaburi 81 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
Au maître de chant. Sur la Gitthienne. D’Asaph. Chantez avec allégresse en l’honneur de Dieu, notre force; poussez des cris de joie en l’honneur du Dieu de Jacob!
2 Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
Entonnez l’hymne, au son du tambourin, de la harpe harmonieuse et du luth!
3 Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
Sonnez de la trompette à la nouvelle lune, à la pleine lune, pour le jour de notre fête.
4 hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
Car c’est un précepte pour Israël, une ordonnance du Dieu de Jacob.
5 Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
Il en fit une loi pour Joseph, quand il marcha contre le pays d’Égypte. J’entends une voix qui m’est inconnue:
6 Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
« J’ai déchargé son épaule du fardeau, et ses mains ont quitté la corbeille.
7 Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
Tu as crié dans la détresse, et je t’ai délivré; je t’ai répondu du sein de la nuée orageuse; je t’ai éprouvé aux eaux de Mériba. — Séla.
8 “Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
« Écoute, mon peuple, je veux te donner un avertissement; Israël, puisses-tu m’écouter!
9 Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
Qu’il n’y ait point au milieu de toi de dieu étranger: n’adore pas le dieu d’un autre peuple.
10 Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
« C’est moi, Yahweh, ton Dieu, qui t’ai fait monter du pays d’Égypte. Ouvre la bouche, et je la remplirai.
11 “Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
« Mais mon peuple n’a pas écouté ma voix, Israël ne m’a pas obéi.
12 Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
Alors je l’ai abandonné à l’endurcissement de son cœur, et ils ont suivi leurs propres conseils.
13 “Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
« Ah! si mon peuple m’écoutait, si Israël marchait dans mes voies!…
14 ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
Bientôt je confondrais leurs ennemis; je tournerais ma main contre leurs oppresseurs.
15 Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
« Ceux qui haïssent Yahweh le flatteraient, et la durée d’Israël serait assurée pour toujours.
16 Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”
Je le nourrirais de la fleur de froment, et je le rassasierais du miel du rocher. »

< Zaburi 81 >