< Zaburi 81 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
To the ouercomer in the pressours of Asaph. Make ye fulli ioye to God, oure helpere; synge ye hertli to God of Jacob.
2 Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
Take ye a salm, and yyue ye a tympan; a myrie sautere with an harpe.
3 Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
Blowe ye with a trumpe in Neomenye; in the noble dai of youre solempnite.
4 hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
For whi comaundement is in Israel; and doom is to God of Jacob.
5 Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
He settide that witnessing in Joseph; whanne he yede out of the lond of Egipt, he herde a langage, which he knew not.
6 Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
He turnede a wei his bak fro birthens; hise hondis serueden in a coffyn.
7 Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
In tribulacioun thou inwardli clepidist me, and Y delyuerede thee; Y herde thee in the hid place of tempest, Y preuede thee at the water of ayenseiyng.
8 “Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
My puple, here thou, and Y schal be witnesse ayens thee;
9 Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
Israel, if thou herist me, a fresche God schal not be in thee, and thou schalt not worschipe an alien god.
10 Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
For Y am thi Lord God, that ladde thee out of the lond of Egipt; make large thi mouth, and Y schal fille it.
11 “Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
And my puple herde not my vois; and Israel yaue not tente to me.
12 Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
And Y lefte hem aftir the desiris of her herte; thei schulen go in her fyndyngis.
13 “Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
If my puple hadde herde me; if Israel hadde go in my weies.
14 ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
For nouyt in hap Y hadde maad low her enemyes; and Y hadde send myn hond on men doynge tribulacioun to hem.
15 Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
The enemyes of the Lord lieden to hym; and her tyme schal be in to worldis.
16 Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”
And he fedde hem of the fatnesse of whete; and he fillide hem with hony of the stoon.

< Zaburi 81 >