< Zaburi 81 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
To the chief Musician upon Gittith, [A Psalm] of Asaph. Sing aloud to God our strength: make a joyful noise to the God of Jacob.
2 Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
Take a psalm, and bring hither the timbrel, the pleasant harp with the psaltery.
3 Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
Blow the trumpet in the new moon, in the time appointed, on our solemn feast day.
4 hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
For this [was] a statute for Israel, [and] a law of the God of Jacob.
5 Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
This he ordained in Joseph [for] a testimony, when he went out through the land of Egypt: [where] I heard a language [that] I understood not.
6 Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
I removed his shoulder from the burden: his hands were delivered from the pots.
7 Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
Thou calledst in trouble, and I delivered thee; I answered thee in the secret place of thunder: I proved thee at the waters of Meribah. (Selah)
8 “Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
Hear, O my people, and I will testify to thee; O Israel, if thou wilt hearken to me;
9 Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
There shall no strange god be in thee; neither shalt thou worship any strange god.
10 Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
I [am] the LORD thy God who brought thee out of the land of Egypt: open thy mouth wide, and I will fill it.
11 “Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
But my people would not hearken to my voice; and Israel would not obey me.
12 Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
So I gave them up to their own hearts lust: [and] they walked in their own counsels.
13 “Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
O that my people had hearkened to me, [and] Israel had walked in my ways!
14 ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
I should soon have subdued their enemies, and turned my hand against their adversaries.
15 Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
The haters of the LORD should have submitted themselves to him: and their time should have endured for ever.
16 Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”
He would have fed them also with the finest of the wheat: and with honey out of the rock I should have satisfied thee.

< Zaburi 81 >