< Zaburi 81 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
To the choirmaster - on the Gittith of Asaph. Sing for joy to God strength our shout for joy to [the] God of Jacob.
2 Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
Lift up music and beat a tambourine a harp pleasant with a lyre.
3 Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
Blow at the new moon a ram's horn at the full moon to [the] day of festival our.
4 hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
For [is] a decree for Israel it an ordinance of [the] God of Jacob.
5 Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
A testimony - in Joseph he established it when went out he on [the] land of Egypt a language [which] not I knew I heard.
6 Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
I removed from a burden shoulder his hands his from a basket they passed away.
7 Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
In trouble you called out and I rescued you I answered you in [the] hiding place of thunder I tested you at [the] waters of Meribah (Selah)
8 “Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
Listen O people my so let me warn you O Israel if you will listen to me.
9 Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
Not it will be among you a god strange and not you must bow down to a god of foreignness.
10 Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
I - [am] Yahweh God your who brought up you from [the] land of Egypt make large mouth your and I will fill it.
11 “Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
And not it listened people my to voice my and Israel not it yielded to me.
12 Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
And I gave over it in [the] stubbornness of heart their they walked in own schemes their.
13 “Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
If people my [will be] listening to me Israel in ways my they will walk.
14 ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
Like a little enemies their I will subdue and on opponents their I will turn hand my.
15 Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
[those who] hate Yahweh They will cringe to him and may it be time their for ever.
16 Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”
And he fed him from [the] best of [the] wheat and from a rock honey I will satisfy you.

< Zaburi 81 >