< Zaburi 81 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
“To the chief musician upon Gittith; by Assaph.” Sing aloud unto God our strength: shout joyfully unto the God of Jacob.
2 Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
Lift up psalm, and bring hither the timbrel, the pleasant harp with the psaltery.
3 Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
Blow on the new moon the cornet, at the time appointed, on the day of our feast.
4 hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
For this is a statute for Israel, an ordinance by the God of Jacob.
5 Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
As a testimony in Joseph did he ordain it, when he went out over the land of Egypt. The language of one I had not known did I hear.
6 Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
I removed from the burden his shoulder: his hands left behind the burden-basket.
7 Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
In distress thou didst call, and I delivered thee; I answered thee in the secret of the thunder: I proved thee at the waters of Meribah. (Selah)
8 “Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
Hear, O my people, and I will give warning unto thee; O Israel, if thou wouldst but hearken unto me!
9 Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
There shall not be among thee a foreign God; nor shalt thou bow thyself down to any strange God.
10 Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
I am the Lord thy God, who have brought thee up out of the land of Egypt: open wide thy mouth, and I will fill it.
11 “Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
But my people did not hearken to my voice; and Israel was not willing [to follow] me.
12 Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
So I let them go in the stubbornness of their own hearts: and they walked in their own counsels.
13 “Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
Oh that my people would hearken unto me, that Israel would walk in my ways!
14 ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
In a little while would I subdue their enemies, and against their adversaries would I turn my hand.
15 Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
The haters of the Lord should offer flattery unto him; but their time should endure for ever.
16 Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”
And he would feed him with the best of wheat: and out of the rock would I satisfy thee with honey.

< Zaburi 81 >